Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 25 Novemba, 2016 katika eneo la Lakilaki nje kidogo ya Jiji la Arusha na kuhudhuriwa na Wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, Viongozi waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kutoka Taasisi na Mashirika ya Umma, Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kwa upande wa Jiji la Arusha pamoja na sehemu ya wakazi wa Arusha.
Rais wa Taasisi ya MICT (Mechanism for International Criminal Tribunal), Jaji Theodor Meron akihutubia wageni waalikwa katika hafla ya uzinduzi wa majengo ya Kisasa ya MICT. |
Mhe. Makamu wa Rais akizungumza wa wakandarasi wa kitanzania ambao walishinda zabuni ya kujenga majengo ya kisasa ya MICT. |
Mhe. Makamu wa Rais akipanda mti katika eneo la majengo ya MICT kwaajili ya uhifadhi wa mazingira. |
Mhe. Waziri Mahiga akipanda mti mbele ya jengo la utawala kwa lengo la kuhifadhi mazingira.pembeni yake ni Msaidizi wake Bw. Gerald Mbwafu na Afisa wa MICT. |
Wazee wa Mila kutoka kabila la Masai, wenyeji wanaoishi jirani na Taasisi ya MICT katika maeneo ya vilima vya Lakilaki wakiliombea baraka eneo la MICT kabla ya zoezi la uzinduzi rasmi. |
Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Baraka Luvanda akifuatilia hotuba. |
Kutoka kulia ni Bw. Gerald Mbwafu pamoja na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kwa makini hafla ya uzinduzi. |
Picha ya pamoja ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Rais wa MICT, Mabalozi kutoka Wizarani na viongozi wengine wa MICT pamoja na Mkandarasi wa majengo ya MICT. |
Picha ya pamoja meza kuu |
Picha ya Pamoja meza kuu na wawakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na MICT |
Mti wa asili unaowakilisha amani (Christmas Tree) ambao ulikuwa umekauka katika eneo la mradi umefanyiwa jitihada za makusudi za kuhudumiwa ili uweze kuota tena. |
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amezindua majengo ya Taasisi mpya ya Kimataifa MICT ambayo inachukua majukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR). Uzinduzi huo umefanyika tarehe 25 Novemba, 2016 katika eneo la Lakilaki Jijini Arusha.
Taasisi hiyo mpya ijulikanayo kama Mfumo wa Kimataifa wa kumalizia Mashauri Masalia ya iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari “international Residual Mechanism for Criminal Tribunal) Imejengwa katika eneo la Lakilaki nje Kidogo ya Jiji la Arusha.
Pamoja na kuendesha Mashauri Masalia ambayo hayakukamilika baada ya ICTR kumaliza muda wake mwaka 2014 pia taasisi hiyo itahifadhi nyaraka za kesi pamoja na kutoa huduma ya maktaba kwa umma hususan katika taaluma ya Sheria ambapo imefanikisha kuanzisha makataba kubwa ya Mfano ya Sheria za Kimataifa katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Mhe. Samia alieleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano itaendelea kutoa ushirikiano wa hali na mali kwa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) katika kuhakikisha Taasisi hii mpya inafanya kazi zake kwa tija ikiwa pamoja na kusimamia Haki za Binadamu, Utawala wa Sheria pamoja na usawa wa jinsia katika nafasi zote unapewa kipaumbele nchini.
“Aidha napenda nimshukuru Msajili wa Taasisi ya MICT, Bw. John Hocking ambaye siku zote ameendelea kujitoa kwa hali na mali katika kusimamia ujenzi wa mradi huu na kuhakikisha unakamilika na kuanza kazi kwa wakati, pamoja na wafanyakazi wote wa MICT” alisema Mhe. Samia.
Aidha, Rais wa MICT Jaji Theodor Meron aliishukuru Serikali ya Tanzania hususan Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambao walikuwa waratibu wakuu katika ufuatiliaji na usimamizi wa mradi sambamba na Taasisi nyingine za Umma kama Shirika la Umeme Tanzani (TANESCO), Mamlaka ya Maji ya Mji Arusha, Ofisi za Jiji la Arusha, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Arumeru pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Shirika la Simu Tanzania (TTCL).
Halikadharika alitoa shukrani za pekee kwa Serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Mstaafu Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Serikali ya awamu ya Tano chini ya Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa ushirikiano waliotoa katika kufanikisha kukamilika kwa mradi.
Jaji Theodor pia alieleza majengo ya Taasisi ya MICT yamejengwa kwa kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 8.78 fedha za nchi wanachama za umoja wa Mataifa na kwamba ardhi kwaajili ya ujenzi ilitolea bure na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sambamba na huduma nyingine zilizokuwa zikiambana na ujezi huo kama maji, umeme, matengenezo ya barabara katika kiwango cha lami ambayo imeitwa "barabara ya haki", huduma ya mtandao na vifaa vya kujengea ambavyo ni rasilimali ya Tanzania na pia ujenzi huo umetumia mkandarasi mzawa kutoka nchini Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ameshukuru Shirika la umoja wa Mataifa kwa maamuzi yake mazuri ya kuipa Tanzania heshima ya kuwa mwenyeji wa Taasisi hiyo na akasema Serikali ya Tanzania itahakikisha haki inasimamiwa katika kesi za kimataifa na akakaribisha mashirika mengine ya Kimataifa kuja kujengwa nchini Tanzania. Pia kwa wale wanaofanya tafiti kuhusiana na Taasisi nyingine za kimataifa ni mahali sahihi kwaajili ya kufanikisha tafiti zao.
Mwaka 2020 Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, lilipitisha Azimio nambari 1966 la kuanzisha Mfumo wa Kimataifa utakaomalizia mashauri ya Masalia kwa zilizokuwa Mahakama za Kimataifa za Mauaji ya Kimbari yaliyotokea nchini Rwanda (ICTR) na Mauaji ya Halaiki yaliyotokea katika iliyokuwa Yugoslavia ya Zamani (ICTY). Katika azimio hilo Baraza kuu la Usalama lilibainisha wazi kwamba Arusha ndiyo itakuwa makao ya Tawi hilo jipya la MICT na The Hague kuwa Makao ya Tawi Jingine.