Quantcast
Channel: Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3230

Balozi Njoolay akabidhi barua ya pongezi kwa Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari

$
0
0
Balozi wa Tanzania, Nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay, alimkabidhi Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari, barua ya pongezi toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete. 
Balozi wa Tanzania, Nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay (kulia) akiwa katika mazungumzo na Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari, mara baada ya kukabidhi barua ya pongezi toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete
Balozi Daniel Ole Njoolay akiendelea kuelezea jambo kwa Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafy Muhammad Buhari mara baada ya kumaliza mazungumzo


====================================

Tarehe 28 Aprili 2015 Balozi wa Tanzania, Nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay, alimkabidhi Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari, barua ya pongezi toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete. 

Rais Mteule Jenerali Buhari alimshukuru Rais Kikwete kwa salamu hizo na kukiri kwamba alikwishapokea simu ya pongezi kutoka kwake mara tu baada ya matokeo kutangazwa. Wakati wa mazungumzo yake na Balozi Njoolay, Generali Buhari aliisifu Tanzania kwa kudumisha amani na utulivu na kusema kuwa anaamini kwamba Tanzania itaendelea kuwa kitovu cha amani na utulivi Barani Afrika. Imetolewa na Ubalozi Tanzania, Abuja

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3230

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>