Quantcast
Channel: Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation
Viewing all 3230 articles
Browse latest View live

TANZANIA, MOROCCO ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO

$
0
0

Tanzania na Morocco zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara na uwekezaji, elimu, utalii, uwezeshaji wa kiuchumi kwa wanawake na vijana.

Makubaliano hayo yamefikiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco Bw. Nasser Bourita walipofanya mkutano wa kwa njia ya mtandao. Balozi Mulamula ameshiriki katika mkutano huo akiwa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

“Tumezungumzia masuala ya kuimarisha uhusiano wetu baina ya Tanzania na Morocco na tumepitia makubaliano yaliyofikiwa wakati wa ziara ya Mfalme wa Morocco alipotembelea Tanzania mwaka 2016 pamoja na kuangalia mikataba mbalimbali iliyotiwa saini wakati wa ziara ya Mfalme wa Morocco ……… laikini pia tumejadili umuhimu wa kuwa na tume ya pamoja ya ushirikiano,” Amesema Balozi Mulamula.

Katika mkutano huo, viongozi hao wamejadili na kukubaliana kuimarisha ushirikiano wa karibu katika sekta za biashara na uwekezaji, utalii, elimu hasa katika kuongeza idadi ya ufadhili wa masomo kwa watanzania kutoka wanafunzi 30 hadi 50.

“Morocco ni nchi inayopata watalii wengi, hivyo tumekubaliana kushirikian kwa karibu zaidi ili kuweza kupata uzoefu ni njia gani wanatumia katika kukuza sekta ya utalii,” ameongeza Balozi Mulamula.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Oman nchini Dkt. Salim Saif Al Harbi katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. 

Mazungumzo ya viongozi hao yamelenga kujadilia masuala mbalimbali ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Serikali ya Tanzania na Oman.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akishiriki mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco Bw. Nasser Bourita. Mkutano huo umefanyika kwa njia ya mtandao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akifuatilia mkutano 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco Bw. Nasser Bourita akimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani) katika mkutano uliofanyika kwa njia ya mtandao 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akimueleza jambo Kaimu Balozi wa Oman nchini Dkt. Salim Saif Al Harbi walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Kaimu Balozi wa Oman nchini Dkt. Salim Saif Al Harbi kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam




TANZANIA NA INDIA KUONGEZA MAENEO YA USHIRIKIANO

$
0
0

Na Mwandishi wetu, Dar

Tanzania na India zimeahidi kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano katika kuhakikisha maendeleo endelevu kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula wakati akihutubia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India jana jioni Jijini Dar es Salaam.

Tanzania na India zimedhamiria kufanya kazi kwa karibu katika kutafuta njia bora ya kufungua fursa mpya na kuimarisha fursa mpya za biashara na uwekezaji zilizopo kati ya nchi hizo.

“Kuanza kwa safari za ndege za moja kwa moja kutoka Dar es Salaam hadi Mumbai kwa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) na kufunguliwa kwa soko la parachichi nchini India ni miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ili kuimarisha na kukuza uhusiano wetu katika sekta za biashara na uwekuzaji pamoja na utalii kati ya India na Tanzania,” Amesema Balozi Mulamula. 

Pamoja na mambo mengine, Balozi Mulamula ameongeza kuwa Tanzania na India kwa sasa zimeanzisha ushirikiano katika usambazaji wa nishati, ujenzi wa miundombinu na Kilimo. Matarajio ya kuimarisha ushirikiano unaoendelea kati ya nchi hizi mbili ni mazuri na yanatia matumaini. 

“Uwekezaji wa India pamoja na idadi ya Wahindi wanaotembelea Tanzania kwa madhumuni ya kuwekeza katika sekta za madini, utalii, viwanda, kilimo, usindikaji wa mazao ya kilimo, nishati, usafirishaji, ujenzi, huduma za fedha na maendeleo ya rasilimali watu unaendelea kuongezeka kwa kasi,” amesema Balozi Mulamula.

Kwa upande wake, Balozi wa India nchini, Mhe. Binaya Srikanta Pradhan amesema kuwa Tanzania imekuwa na uhusiano mzuri na India ambapo uhusiano huo umekuwa ni chachu ya maendeleo kwa mataifa yote mawili na umepelekea kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano.

“Ushirikiano na mshikamano uliopo baaina ya mataifa yetu mawili umekuwa chachu ya maendeleo na lengo la ushirikiano wetu yetu ni kukuza uchumi wetu,” amesema Balozi Pradhan 

Aidha, Balozi Pradhan amebainisha kuwa Tanzania itaendelea kuwa ya kipekee kwa taifa la India kutokana na mshikamano ambao umepelekea mataifa haya kufanya biashara, uwekezaji, kujenga uwezo, ujenzi wa miundiombinu pamoja na maendeleo ya kiuchumi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akihutubia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India jana jioni Jijini Dar es Salaam

Balozi wa India nchini, Mhe. Binaya Srikanta Pradhan akihutubia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India jana jioni Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula. 

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Kiongozi wa Mabalozi nchini ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed 

Sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India zikiendelea jana jioni Jijini Dar es Salaam

Balozi Mulamula na baadhi ya Mabalozi wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India jana jioni Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India jana jioni Jijini Dar es Salaam

Sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India jana jioni Jijini Dar es Salaam

Mabalozi na wageni waalikwa wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India  

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya 73 ya Jamhuri ya India  


MKUTANO WA 19 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA AFRIKA NA NORDIC KUFANYIKA JUNI 2022 FINLAND

$
0
0

Na Mwandishi Wetu, Dar

Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Afrika na nchi za Nordic unatarajiwa kufanyika mwezi Juni 2022 nchini Finland.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Finland nchini Mhe. Riitta Swan leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Katika kuendeleza na kuimarisho ushirikiano wa nchi hizo mbili viongozi hao wamependekeza kufanikisha ziara ya Mhe. Waziri Mulamula nchini Finland pamoja na ushiriki wake katika mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Nordic utakaofanyika nchini Finland mwezi Juni 2022. 

Katika mazungumzo ya viongozi hao, Balozi Mulamula amemhakikishia Balozi Swan kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na Finland katika kuhakikisha Mataifa hayo yanashirikiana kijamiii, kisiasa na kiuchumi.

"Finland amekuwa mdau Mkubwa wa Maendeleo hapa nchini kwetu hasa katika sekta ya fedha hususan katika masuala ya kodi, mazingira, tehama, uongozi pamoja na uwezeshaji wa wanawake........pia tumekubaliana kuendeleza ushirikiano wetu kwa Maendeleo endelevu," amesema Balozi Mulamula.

Katika tukio jingine, Waziri Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Benki ya Stanbink Tanzania Bw. Kevin Wingfield
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika mazungumzo na Balozi wa Finland nchini Mhe. Riitta Swan leo katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiteta jambo na  Balozi wa Finland nchini Mhe. Riitta Swan pamoja na Afisa kutoka Ubalozi wa Finland nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Balozi wa Finland nchini Mhe. Riitta Swan, wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki Balozi Swahiba Mndeme, Bi. Kisa Mwaseba Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Afisa kutoka Ubalozi wa Finland 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Benki ya Stanbink Tanzania Bw. Kevin Wingfield yaliyofanyika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam



TANZANIA NA MAURITIUS ZASAINI MKATABA WA JUMLA

$
0
0

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Mauritius zimesaini Mkataba wa Jumla (General Framework Agreement - GFA)

Mkataba huo umesainiwa na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Mauritius mwenye makazi yake Harare Zimbabwe Mhe. Prof. Emmanuel Mbennah pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa ya nchini Mauritius Mhe. Balozi Haymandoyal Dillum na kushuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa Mhe. Alan Ganoo  

Mkataba huo pamoja na mambo mengine utaimarisha uhusiano wa kiuchumi, kisayansi na kiutamaduni. Mkataba huo pia utaanzisha Tume ya Pamoja ya Kudumu baina ya Nchi itakayokuwa ikifuatilia utekelezaji wa masuala mbalimbli kuhusu ushirikiano wa Tanzania na Mauritius. Hafla ya Uwekaji saini ilihudhuriwa pia na Viongozi wa Serikali na Taasisi kutoka Sekta Binafsi.

Aidha, kwa nyakati tofauti Balozi Mbennah alikutana kwa mazungumzo na Waziri mwenye dhamana na masuala ya Biashara Mhe. Soodesh Satkam Callichurn na Waziri mwenye dhamana na masuala ya Viwanda Mhe. Soomilduth Bholah. 

Mazungumzo na viongozi hao yalijikita katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi ili Tanzania na Mauritius ziweze kunufaika na fursa zilizopo katika Nchi hizo.

Balozi waTanzania nchini Mauritius Mhe. Prof. Emmanuel Mbennah pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa ya nchini Mauritius Mhe. Balozi Haymandoyal Dillum wakisaini Mkataba wa Jumla (General Framework Agreement - GFA) na kushuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa Mhe. Alan Ganoo

Balozi waTanzania nchini Mauritius Mhe. Prof. Emmanuel Mbennah katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa ya nchini Mauritius Mhe. Balozi Haymandoyal Dillum na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa Mhe. Alan Ganoo mara baada ya kusaini Mkataba wa Jumla (General Framework Agreement - GFA) 

Balozi waTanzania nchini Mauritius Mhe. Prof. Emmanuel Mbennah akibadilishana Mkataba wa Jumla na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Biashara za Kimataifa ya nchini Mauritius Mhe. Balozi Haymandoyal Dillum  

Balozi wa Tanzania nchini Mauritius Prof. Emmanuel Mbennah akizungumza na Waziri Mkuu Mhe. Pravind Kumar Jugnauth, ambapo Mhe. Jugnauth ameipongeza Tanzania na Mauritius kuweka saini Mkataba wa Jumla ambao utaongeza wigo wa ushirikiano kwa nchi hizo mbili 


BALOZI MULAMULA: MISINGI YA SERA YA MAMBO YA NJE HAIJABADILIKA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amesema kuwa Misingi ya Sera ya Mambo ya Nje haijabadilika na iko imara, kusisitiza umoja na kutoshabiana kisiasa na upande wowote pamoja na kuwaunga mkono wale wote wanaokandamizwa.

Balozi Mulamula ameyasema hayo wakati alipokutana katika kikao kazi na watumishi wa Wizara ya leo Jijini Dodoma na kuwasihi watumishi kujenga mahusiano na kutekeleza kwa ufanisi Diplomasia ya Uchumi.

“Uchumi wa Tanzania unakuwa kutokana na juhudi zetu, na mtakumbuka kuwa Wizara ya Mambo ya Nje majukumu yake ni mtambuka kwani yanagusa kila sekta, na lengo la kikao hiki ilikuwa kukumbushana maagizo ya Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,”

“Nashukuru sana katika kukutana kwenye kikao na wafanyakazi binafsi nimehamasika na kuwa na ari mpya ya kuchapa kazi, na pia wafanyakazi wamehamasika mara baada ya kikao cha leo,” 

Katika awamu ya Sita, Serikali imefungua balozi mbili mpya na Konseli mbili na naamini kutokana na msisitizo wa Mhe. Rais Samia wa kutekeleza Diplomasia ya uchumi kwa vitendo tutaendelea kufungua balozi nyingine zaidi kadri tutakapokuwa tunapata uwezo…….kile tulichonacho tukitumie vizuri kwani milango imefunguka.

Mazingira ni mazuri na ndiyo maana tunaendelea kuhamasisha wawekezaji na wafanyabiashara kuja kuwekeza Tanzania.

Mwana Diplomasia namba moja Mhe. Rais Samia amekuwa mstari wa mbele kutusaidia katika hili na hata juzi alipokutana na mabalozi na wakuu wa mashirika ya kimataifa aliweza kuwaeleza kuwa Tanzania ipo pamoja na kwamba tunaenda wote katika kufanikisha malengo ya watanzania yaweze kuboreka Zaidi.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Nassor Mbarouk (Mb), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine pamoja na Naibu katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) akifurahia jambo alipokuwa akizungumza na Watumishi wa Wizara jijini Dodoma
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Nassor Mbarouk (Mb), akizungumza na watumishi wa Wizara kwenye kikao kilichofanyika jijini Dodoma 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akizungumza na watumishi wa Wizara kwenye kikao kilichofanyika jijini Dodoma 

Kutoka kushoto; Naibu katibu Mkuu Mhe. Balozi Fatma Rajab, Naibu Waziri Mhe. Balozi Nassor Mbarouk (Mb), Waziri Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Mkurugenzi Msaidizi Menejimenti ya Rasilimali Watu Bw. Peter Bunyazu wakiwa kwenye kikao na Watumishi wa Wizara kilichofanyika jijini Dodoma
Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo (mstari wa mbele) wakifuatilia Kikao kilichokuwa kikiendelea baina Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na watumishi wa Wizara.
Kikao kikiendelea

Kikao kikiendelea

Picha ya pamoja Meza Kuu na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Picha ya pamoja Meza Kuu na Wakuu wa Taasisi zilipo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Picha ya pamoja Meza Kuu na baadhi ya Watumishi wa Wizara

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA ALFA CARE GROUP LIMITED

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kati) amekutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Alfa Care Group Limited Bw. Dadkarim Mulla (wa kwanza kushoto) ambaye aliambatana na  Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Mrisho Gambo (wa pili kushoto) walipomtembelea Wizarani tarehe 1 Februari 2022 jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Edwin Rutageruka (mwenye tai) na Katibu wa Waziri, Bw. Seif Kamtunda.

Katika Mazungumzo yao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi kwa lengo ya kuyafikia malengo ya kitaifa kwa ufanisi.

Vilevile wamejadili namna ya kuongeza uwekezaji katika miradi ya maendeleo husasani sekta ya afya, miundombinu, teknolojia, utalii sambamba na kukuza ajira kwa watanzania.

Mazungumzo yakiendelea.

Picha ya pamoja
Mhe. Balozi Mulamula akimkabidhi Mhe. Gambo Calenda na Shajara za Wizara.

Mhe. Waziri akimkabidhi pia Bw. Mulla calenda ya Wizara

 

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA BALOZI WA MAREKANI NCHINI

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Donald Wright leo tarehe 2 Februari 2022 jijini Dodoma.
Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani katika sekta za afya, uwekezaji, biashara na uhusiano wa kimataifa. 


Kushoto ni afisa kutoka Ubalozi wa Marekani, Bi. Kristin Mencer akifuatilia mazungumzo.

Kutoka kulia ni Katibu wa Waziri, Bw. Seif Kamtunda na Afisa Mambo ya Nje Bi. Talha Waziri wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea.

Picha ya Pamoja.



 

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA SAUDIA ARABIA

$
0
0

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.Kikao hicho kilifanyika ofisini kwa Mhe. Waziri Mttumba jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia (walioko kushoto) wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini (katikati) katika kikao na Wawekezaji kutoka nchini Saudi Arabia(hawapo pichani) kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Hemedi Mgaza na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi Balozi Edwin Rutageruka wakati wa kikao na wawkezaji hao



Waziri Mulamula (katikati) katika picha ya pamoja na ujumbe wa  wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia waliokuja nchini kuangalia fursa za biashara na uwekezaji baada ya kumalizika kwa kikao chao jijini Dodoma

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini akiwa nje ya jengo la Wizara katika Mji wa Serikali Mtumba akizungumza na wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia aliokuja nao Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji baada ya kumalizika kwa kikao chao na Mhe Waziri Mulamulajijini Dodoma


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka Kiwanda cha Pioneers Chemical Factory cha nchini Saudi Arabia wanaotembelea Tanzania kuangalia fursa za biashara na uwekezaji.

 

Mhe. Waziri Mulamula amekutana na Ujumbe wa wawekezaji hao ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma leo tarehe 02 February 2022. Ujumbe wa wawekezaji hao umeongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Saudia Arabia Mhe. Ali Mwadini umeelezea utayari wao wa kuja kuwekeza nchini.

Akizungumza katika kikao hicho Balozi Mulamula amewakaribisha wawekezaji hao na kuwahakikishia mazingira rafiki ya uwekezaji nchini na kwamba Tanzania iko tayari kuwapokea.

Amesema Tanzania na Saudia zina uhusiano wa muda mrefu ambao una historia ya aina yake na kwamba uwekezaji kutoka kwa kampuni hiyo ni sehemu ya kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia.

Kampuni hiyo inayomiliki viwanda mbalimbali nchini Saudi Arabia inajishughulisha na uzalishaji wa pembejeo za Killimo hususan, mbolea za kupandia na kukuzia mimea pamoja na dawa (pesticides) aina ya ‘phosphorus, nitrogen, potassium na sulfur’.

Mbali na uzalishaji wa mbolea na dawa, Kampuni hiyo pia inazalisha vifaa vya kilimo vya plastiki ikiwa ni pamoja na khusambaza bidhaa katika nchini za Saudi Arabia, ukanda wa Mashariki ya Kati na duniani kote.

 

Wawekezaji hao waliwasili nchini Januari 28, 2022  wametembelea Mikoa ya Mtwara, Lindi Mtwara na Dodoma na kukutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Mikoa hiyo, wadau wa sekta binafsi na wakulima wa korosho kuzungumzia biashara na uwekezaji katika nyanja hizo. 

Wawekezaji hao wamemuhakikishia Mhe. Waziri Mulamula juu ya nia yao ya kuja kuwekeza Tanzania na kutaja maeneo ambayo ni kipaumbele chao kuwa ni madini, biashara, kilimo na mifugo

 


WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA UJUMBE WA SERIKALI YA URUSI

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Masuala ya Kibinadamu kutoka nchini Urusi Bw. Yevgeny Primakov leo tarehe 03 Februari 2022 katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Bw. Primakov ameambatana na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Yuri Popov pamoja na Mjumbe kutoka Serikali ya Urusi, Bw. Egor Utkin.

Wawakilishi hao kutoka Serikali ya Shirikisho la Urusi waliwasilisha ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimirovich Putin.

Pamoja na mambo mengine viongozi hao walijadili juu ya kuimarisha ushirikiano uliopo na kwamba kwa sasa Tanzania na Urusi zinajikita zaidi katika kufungua maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii na masuala mengine ya kiuchumi kwa maslahi mapana ya mataifa hayo.

Waziri Mulamula alieleza kuwa Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano mzuri na wa kihistoria ambao uliasisiwa na Waasisi wa Mataifa hayo mawili.  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kushoto) akipokea ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia)kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimirovich Putin

Mazungumzo yakiendelea. 

Picha ya pamoja Mhe. Waziri na Ujumbe kutoka Serikali ya Urusi.
Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme, na Kulia kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mhe. Fredrick Kibuta.
 Kutoka kulia kwa Mhe. Waziri ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Urusi, Bw. Evgeny Primakov, Balozi wa Urusi nchini,
 Mhe. Yuri Popov pamoja na Mjumbe kutoka serikali ya Shirikisho la Urusi, Bw. Egor Utkin.

Waziri Mulamula akikabidhi shajara.
                                                                                      
Picha ya Pamoja.

MAAFISA JWTZ WATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ITALIA

$
0
0

Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakiongozwa na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira pamoja na Col. Abdallah Khalfan wametembelea Ubalozi wa Tanzania Jijini Roma, Italia.

Wakiwa Ubalozini walipokelewa na mwenyeji wao Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo ambapo pamoja na mambo megine wamezungumzia masuala ya ushirikiano. Maafisa hao walikuwepo nchini Italia kwa shughuli za kikazi. 

Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira katika ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Italia 


Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira na Col. Abdallah Khalfan   


Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Mkuu wa Kurugenzi ya Intelijensia Makao Makuu ya Jeshi, Maj. Gen. Ramadhani Mrangira, Col. Abdallah Khalfan pamoja na baadhi ya watumishi wa Ubalozi    


 

FURSA ZA AJIRA NA USHAURI ELEKEZI KATIKA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA

$
0
0
Fursa za ajira na ushauri elekezi kwa Watanzania katika benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)



 

WAZIRI MULAMULA: TUTAENDELEA KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA NISHATI NCHINI

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula amesema Wizara kwa kushirikiana na Wizara zingine, Mashirika na Taasisi za Serikali na Sekta binafsi itaendelea kuweka jitihada katika kutangaza fursa za uwekezaji zinazotokana na sekta ya nishati. 

Waziri Mulamula ameeleza haya wakati wa mazungumzo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ocean Business Partners Tanzania Ltd Bw. Abdulsamad Abdulrahim na Makamu wa Rais, wa Kampuni ya dmg event ya nchini Uingereza Bw. Damian Howard yaliyofanyika Ofisini kwake jijini Dodoma. “Licha ya hazina kubwa tuliyonayo katika sekta ya nishati, serikali pamoja sekta binafsi bado tunakazi kubwa ya kuendelea kutangaza na kutafuta wawekezaji ili kukuza uwekezaji na mapato katika sekta hii. Waziri Mulamula. 

Bwana Abdulsamad na Bw. Howard wamepongeza juhudi zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi madhubuti wa Mhe.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini. Waliongeza kusema Makampuni yao yataendelea kuunga mkono jitihada za serikali katika kutangaza fursa za uwekezaji zinazotokana na sekta ya nishati nje ya mipaka ya Tanzania. 


Katika tukio jingine Waziri Mulamula amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Adam Malima alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma. 

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Edwin Rutageruka (wa kwanza kusho), Mkurugenzi wa Diplomasia Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje, Makamu wa Rais wa Kampuni ya dmg event ya nchini Uingereza Bw. Damian Howard (wa pili kushoto) na Bw. Abdulsamad Abdulrahim (kulia) Mkurugenzi wa Kampuni ya Ocean Business Partners Tanzania Ltd walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.
Mazungumzo yakiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Adam Malima wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Adam Malima wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma

WAZIRI MULAMULA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA 46 WA DHARURA WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, akiwa jijini Dodoma ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki katika Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Mkutano huu wa dharura umeitishwa kwa lengo la kujadili ripoti ya majadiliano yaliyofanyika tarehe 15 hadi 24 Januari 2022 jijini Nairobi, Kenya kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuhusu Nchi hiyo kujiunga na Jumuiya. 

Pamoja na muasula mengine yaliyojadiliwa Mkutano umekubaliana kuendelea kufanyia kazi kwa wakati hoja za pande zote mbili za majadiliano (EAC na Congo DRC), na kuandaa taarifa itakayowasilishwa kwa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ili kuharakisha uridhiaji wa maombi ya DRC

Mkutano huu wa dharura ambao umefanyika kwa njia ya mtandao umehudhuriwa na Nchi zote wanachama wa Jumuiya na kuongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Waziri anayesimamia masuala ya Mtangamano wa Afrika Mashariki Mhe. Adam Mohamed kutoka nchini Kenya. 

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliwasilisha maombi ya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki tarehe 4 Juni 2019. 
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine (katika) na Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama Balozi Stephen Mbundi wa Wizara hiyo wakifuatilia Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliokuwa ukiendelea
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliokuwa ukiendele
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea kwenye Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akichangia hoja kwenye Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika kwa njia ya mtandao.

MKUTANO WA 15 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA KISEKTA LA NISHATI LA EAC WAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA KATIKA NGAZI YA WATAALAMU

$
0
0

Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki umefunguliwa leo tarehe 8 Februari 2022 jijini Arusha, Tanzania katika ngazi ya Wataalamu.


Mkutano huu utafanyika katika ngazi tatu ambapo umeanza na; Mkutano Ngazi ya Wataalamu unaofanyika tarehe 8 hadi 9 Februari 2022, utafuatiwa na Mkutano Ngazi wa Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 10 Februari 2022 na utamalizika kwa Mkutano Ngazi ya Mawaziri utaofanyika tarehe 11 Februari 2022.


Lengo la Mkutano huu ni kupitia na kuandaa taarifa ya hali ya utekelezaji wa Maamuzi/Maagizo ya mikutano iliyopita; Hatua iliyofikiwa hadi sasa katika sekta za Nishati Umeme, Nishati Mafuta, na Nishati Jadidifu; pamoja na Utekelezaji wa Miradi/Programu mbalimbali za Kitaifa na Kikanda ya Sekta za Nishati inayotekelezwa ndani ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.


Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano Ngazi ya Wataalamu unaongozwa na Kamishna Msaidizi Maendeleo ya Umeme kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila ambaye ameambatana na Mkurugenzi Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota, Mkurugenzi Idara ya Nishati na Madini kutoka Wizara ya Nishati na Madini Zanzibar, Mhandisi Said H. Mdungi pamoja na maafisa wengine Waandamizi kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye dhamana katika sekta ya nishati.


Mkutano Ngazi ya Wataalamu na Ngazi ya Makatibu Wakuu ni sehemu ya mikutano ya awali kwaajili ya maandalizi ya Mkutano wa  Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki utaofanyika tarehe 11 Februari 2022. 


Kushoto ni Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania katika Mkutano Ngazi ya Wataalamu na Kamishna Msaidizi wa Maendeleo ya Umeme katika Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akifafanua jambo wakati wa majadiliano ya mkutano huo.

Mwenyekiti wa Mkutano Ngazi ya Wataalamu na Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu kutoka Jamhuri ya Kenya, Mhandisi Benson Mwakina (Kushoto) akiongoza majadiliano, kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Sekta za Uzalishaji na Jamii, Bw. Christophe Bazivamo. 

Kushoto ni Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Mgeta Sabe na wajumbe wengine wa Tanzania wakifatilia majadiliano.
Mkutano ukiendelea

Ujumbe wa Tanzania.

Sehemu nyingine ya Ujumbe wa Tanzania.



RAIS WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AFDB) DKT. ADESINA AWASILI DODOMA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akisalimiana naRais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki BaloziLiberata Mulamula (katikati) akizungumza na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina (kushoto) huku Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia) akiwasikiliza wakati Dkt. Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.


Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina (wa pili kushoto) akizungumza na wenyeji wake waliompokea katika Uwanja wa ndege Dodoma alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma huku Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (kulia) wakifuatilia mazungumzo hayo.




Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina awasili jijini Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini. Katika uwanja wa ndege wa Dodoma Dkt. Adesina amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba.

Dkt. Adesina yuko nchini kwa ziara ya siku tatu ambapo tarehe 09 February 2022 atashiriki katika uzinduzi wa ujenzi wa barabara za mzunguko zinazojengwa katika jiji la Dodoma utakaofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Ujenzi wa barabara hizo za mzunguko zenye urefu wa kilomita 112.3 unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na benki hiyo. Ujenzi wa barabara hizo utalifanya jiji la Dodoma kuwa na barabara za aina yake katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.


VACANCY ANNOUNCEMENT

WATANZANIA WAASWA KUILINDA NCHI

$
0
0
Imeelezwa kuwa jukumu la kulinda nchi ni la kila Mtanzania na vijana wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kwa kuwa wao ni chachu ya ukuaji uchumi wa nchi na viongozi watarajiwa wa Taifa hili.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola wakati alipokuwa anafungua semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma.

Balozi Kayola alisema Wizara imekuwa na utaratibu wa kutoa elimu kwa wanafunzi ili wao kama vijana wawe na elimu stahiki kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa ambayo yatawawezesha kushiriki kikamilifu katika kutumia fursa za mtangamano ukiwemo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ( EAC).

Alieleza kuwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, vijana wametambuliwa kama kundi muhimu kwa maendeleo ya jumuiya hiyo, hivyo utoaji wa elimu hiyo ni muhimu ili vijana wafahamu fursa zilizopo katika nyanja mbalimbali za uchumi, utamaduni, elimu na siasa na namna na ya kuzichangamkia. 

Aliwambia wanafunzi hao kuwa Sera ya Vijana ya EAC imeweka bayana haki za vijana kuwa na uhuru wa kutembea na kuweka makazi kwenye nchi yoyote ya Jumuiya kwa madhumuni mbalimbali kama kutafuta elimu, ajira au kufanya biashara, hivyo ni muhimu kwa vijana hao wanapoelekea kuhitimisha masomo yao ya sekondari ni vyema wakaweka mipango ya kuchangamkia furza za EAC.

Balozi Kayola alihitimisha hotuba yake kwa kuwasihi vijana hao kuwa mabalozi waźuri wa Tanzania katika safari yao ya maisha na kuwaelimisha wanafunzi wenzao na jamii kwa ujumla ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kupata elimu hiyo.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imejiwekea utaratibu wa kuelimisha makundi mbalimbali katika Jumuiya yakiwemo ya wanafunzi kuhusu Sera ya Mambo ya Nje. Na katika semina hiyo wanafunzi hao walielimishwa kuhusu majukumu ya Wizara, utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje, hatua za mtangamano wa EAC na fursa zake pamoja mchakato wa kuelekea shirikisho la kisiasa la EAC.

Semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma masuala mbalimbali ya Mtangamo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiendelea 

Sehemu ya wadau wakifuatilia semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma iliyofanyika kwenye ukumbi wa informatics katika Chuo Kikuu cha Dodoma

Picha ya patoja
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Balozi Agness Kayola akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Bw. Emmanuel Buhohela. Wote kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Semina ikiendelea
Semina ikiendelea

MAKATIBU WAKUU WA SEKTA YA NISHATI WA EAC WAMEKUTANA JIJINI ARUSHA

$
0
0
Makatibu Wakuu wa sekta ya nishati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamekutana leo tarehe 10 Februari 2022 jijini Arusha, Tanzania.

Mkutano wa Makatibu Wakuu ulitanguliwa na mkutano wa Maafisa Waandamizi uliofanyika tarehe 8 na 9 Februari 2922. Hii ni mikutano ya awali kwaajili ya maandalizi ya Mkutano wa 15 Wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika kesho tarehe 11 Februari 2022.


Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Makatibu Wakuu umeongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati (Tanzania Bara), Mhandisi Felchesmi Mramba ambaye ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini wa Zanzibar, Dkt. Mngereza Miraji.


Pamoja na mambo mengine Mkutano wa Makatibu Wakuu umepitia na kuandaa: Taarifa ya hali ya utekelezaji wa maagizo ya mikutano iliyopita; Hatua iliyofikiwa hadi sasa katika sekta za Nishati Umeme, Nishati Mafuta, na Nishati Jadidifu; pamoja na Utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Kitaifa na Kikanda ya Sekta za Nishati inayotekelezwa ndani ya Jumuiya ya Afrika  Mashariki.


Akiongea wakati wa ufunguzi wa mkutano mwenyekiti wa mkutano huo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati wa Jamhuri ya Kenya, Maj. Gen. Dkt. Gordon Kihalangwa, CBS alieleza kuwa uhaba wa nishati ndani ya nchi zetu na jumuiya kwa ujumla huleta changamoto kwa wananchi wote na kushusha shughuli za uchumi na pato la taifa kwa ujumla. Hivyo, akasisitiza umuhimu wa kuunganisha nguvu katika kutekeleza miradi ya nishati ya kitaifa na kikanda.


Vilevile akaeleza umuhimu wa sekta ya afya kupatiwa nishati ya kutosha na ya uhakika ili kuondoa changamoto za mara kwa mara zinazochangia kukosekana kwa huduma hizo.


 “Huduma za mama na mtoto pamoja na huduma nyingine za afya ni muhimu zikazingatia upatikanaji wa nishati ili kupunguza matatizo yatokanayo na kukosekana kwa nishati ya uhakika kwa baadhi ya vifaa vinavyohitaji nishati ya umeme na gesi” alisema Dkt. Gordon.


Mkutano huu umefanyika kwa njia ya mseto ambapo nchi za Tanzania, Kenya na Uganda wameshiriki mkutano wa ana kwa ana isipokuwa Burundi, Rwanda na Sudan Kusini wameshiriki kwa njia ya mtandao.

 

Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri  la Kisekta la Jumuiya ya Afrika Mashariki la Nishati na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati (Tanzania Bara) akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini (Tanzania Zanzibar), Dkt. Mngereza Miraji wakifuatilia majadiliano kwenye mkutano huo.

Mwenyekiti wa Mkutano huo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati wa Jamhuri ya Kenya, Maj. Gen. Dkt. Gordon Kihalangwa, CBS (kati) akifungua Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika tarehe 10 Februari 2022 jijini Arusha, Tanzania. Kushoto ni Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati waJamhuri ya Kenya, Mhandisi Benson Mwakina. 

Kulia ni Mkurugenzi Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akifuatilia majadiliano katika mkutano huo.

Kutoka kushoto Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Mgeta Sabe na Mhandisi Emmanuel Yessaya kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wakifuatilia majadiliano.

Ujumbe wa Tanzania

Mkutano ukiendelea

Ujumbe kutoka Uganda

Ujumbe kutoka Kenya


Balozi Kilima ateta na Wawekezaji kutoka Ujerumani

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima amefanya mazungumzo na wawekezaji wa nishati ya jua kutoka Oman jijini Muscat hivi karibuni.
Wawekezaji hao ambao ni Dkt. Michael Voch na Bw. Claus Heim kutoka Ujerumani na Bw. Khalid Hamdoun M. Aljabri  na Bw. Mohammed Al Riyami kutoka Taasisi ya  IGD ya Oman wanakusudia kuwekeza katika sekta ya uzalishaji wa nguvu ya umeme wa kutumia Jua kwa teknolojia mpya inayoitwa Solar Container. Teknolojia hiyo inatumua maji kuzalisha hydrojen ambayo ndiyo inayotoa umeme na oxygen kama mabaki ya uzalishaji (byproducts)
Teknolojia hiyo tayari inatumika katika nchi za Ulaya na hivi karibuni itaanzishwa nchini Oman inaweza kutosheleza nyumba 200 Kwa kontena moja na pia inaweza kuunganishwa na Gridi ya Taifa
Wawekezaji hao pia wanakusudia kuanzisha miradi ya kilimo inayotumia Teknolojia ya Hydroponic system ambacho kinatunia eneo dogo lakini tija kubwa.
Wawekezaji imeiomba Serikali ya Tanzania kuwapatia eneo la uwekezaji pamoja na kuunganishwa na makampuni yatakayoweza kununua bidhaa watakazozalisha kama wanavyofanya nchini UAE, waneingia mkataba na Shirika la Ndege la Emirate kununua bidhaa za vyakula watakavyozalisha.
Kwa upande wake, Mhe. Balozi aliwaeleza wawekezaji hao kwamba Tanzania inakarubisha uwekezaji katika sekta ya uzalishaji wa nguvu za umeme wa kutumia Jua kwani ni nishati mbadala na rahisi kutumika. Kwa upande wa mradi wa kilimo cha hydroponic, Mhe. Balozi alieleza kwamba kilimo hicho kinaweza kuwa mkombozi wa kilimo cha kutegemea mvua ambacho huwa ni cha msimu. Hivyo mradi huo unaweza kuongeza uzalishaji na kupata ziada ya kuuza nje ya nchi. 

Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima akizungumza na wawekezaji kutoka Ujerumani. Kulia Kwake ni Dkt. Michael Voch na Bw. Claus Heim

 

MAWAZIRI WA SEKTA YA NISHATI WA EAC WASISITIZA UMUHIMU WA KUPATIKANA KWA NISHATI YA UHAKIKA

$
0
0

Mawaziri wa Sekta ya Nishati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamekutana leo tarehe 11 Februari 2022 jijini Arusha, Tanzania kwa lengo la kuhudhuria Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya hiyo.

Mkutano huu ulitanguliwa na mikutano ya awali ngazi ya Wataalamu/Maafisa waandamizi uliofanyika tarehe 8 na 9 Februari 2022 na kufuatiwa na mkutano ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 10 Februari 2022.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huu umeongozwa na Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (Mb.) ambaye ameambatana na; Katibu Mkuu Wizara ya Nishati - Tanzania Bara, Mhandisi Felschesmi Mramba; Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini -Zanzibar; Dkt. Mngereza Miraji; Mkurugenzi Mtendaji Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio; Kamishna wa Petroli na Gesi kutoka Wizara ya Nishati; Bw. Michael Mjinja na Maafisa Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa ujumla.

Akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Waziri Makamba aliwakaribisha nchini wajumbe wa mkutano huo na kuwahakikishia kuwa mkutano utafanikiwa kuyafikia malengo yake kufuatia uongozi imara wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Peter Mathuki.

Vilevile akaeleza ukanda wa Afrika Mashariki umejaaliwa rasilimali nishati za kutoka hivyo, ni wakati sasa kwa kila nchi kuwa na mikakati imara ya kuhakikisha nishati ya uhakika inapatikana ili kuihakikishia jamii upatikanaji wa huduma zote zinazohitaji nishati.

“Tukiwa tunapitia changamoto za ugonjwa wa COVID-19 tumeshuhudia namna gani nishati zilihitajika katika kusaidia kuleta nafuu na kuokoa maisha ya wananchi wetu” alisema Mhe. Makamba.

Naye mwenyekiti wa mkutano huo na Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. Monica Juma alitumia nafasi hiyo kuwashukuru Watalamu na Makatibu Wakuu kwa kufanya maandalizi mazuri ya Mkutano huo na kusisitiza kuwa upatikanaji wa umeme wa uhakika ni moja ya viashiria vya kukua kwa uchumi wa nchi yeyote.

Pia akaeleza kukua kwa uchumi husaidia kupunguza utegemeze na hivyo jitihada za makusudi zinahitajika kuziwesha Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kufanya uzalishaji wa kutosha viwandani na katika sekta ya kilimo.

Mkutano huu wa 15 wa Baraza la Mawaziri wa Kisekta la Nishati pamoja na mambo mengine utapitia na kutoa maamuzi juu ya; Tarifa ya hali ya utekelezaji wa maagizo ya mikutano iliyopita; Hatua iliyofikiwa hadi sasa katika sekta za Nishati Jadidifu, Nishati ya Umeme na Nishati ya Mafuta; pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Kitaifa na Kikanda ya Sekta za Nishati inayotekelezwa ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kadhalika mkutano huu utajadili kwa kina utekelezaji wa mradi wa kituo cha Nishati Jadidifu cha Afrika Mashariki; Mradi wa Kufua Umeme wa Nsongezi; Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kigagati (14MW) na Taasisi ya Mamlaka ya udhibiti wa Nishati katika Nchi za Afrika Mashariki.


===================================================

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika leo tarehe 11 Februari 2022 jijini Arusha Tanzania.

Picha ya pamoja meza kuu; Wapili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Mkutano na Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Monica Juma akiongoza mkutano huo, kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Peter Mathuki na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia Sekta za Uzalishaji na Jamii, Bw. Christophe Bazivamo na mwisho kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati kutoka Jamhuri ya Kenya Mej. Gen. Dr. Gordon Kihalangwa wakifatilia mkutano.

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (wa pili kutoka kushoto) pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati (Tanzania Bara), Mhandisi Felschemi Mramba (wa kwanza kushoto); Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini -Zanzibar, Dkt. Mngereza Miraji (wa pili kulia ) na Kamishna wa Petroli na Gesi Wizara ya Nishati, Bw. Michael Mjinja (wa kwanza kulia )wakifatilia mkutano. 

Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akifuatilia majadiliano wakati wa mkutano huo.

Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania (TPDC) Dkt. James Mataragio na Kamishna Msaidizi Maendeleo ya Umeme kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila wakifuatilia majadiliano. 

Maafisa Waandamizi kutoka Wizara za Nishati Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.

Maafisa Waandamizi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)

Kutoka kushoto ni Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhandisi Mgeta Sabe pamoja na maafisa waandamizi kutoka Taasisi za Nishati wakifuatilia mkutano 

Ujumbe kutoka Kenya

Ujumbe kutoka Uganda


Viewing all 3230 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>