Quantcast
Channel: Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation
Viewing all 3230 articles
Browse latest View live

PRESS RELEASE

$
0
0
H.E. Ram Baran Yadav, President of Nepal

PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a condolence message to H.E. Ram Baran Yadav, President of the Democratic Republic of Nepal following a tragic earthquake that rocked Nepal on Saturday 25 April 2015.

The message reads as follows:

“H.E. Ram Baran Yadav,
President of the Federal Democratic Republic of Nepal,
KATHMANDU

I have learnt with profound shock and deep sorrow the sad news of a 7.8 magnitude earthquake that hit Nepal on Saturday, 25 April 2015 claiming at least 1,800 lives and devastating buildings and centuries old temples.

The tragedy is not only for the loved ones of those who perished but also for all the Nepali people and their friends. As a country therefore, our thought and prayers are with the people of Nepal in this time of grief.

On behalf of the Government and the People of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, I offer deep condolences to the victims of the powerful earthquake and also sincere sympathies to the injured and families of the victims.

Please accept, Your Excellency, the assurances of my highest consideration”.

ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

27TH APRIL, 2015




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

$
0
0
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

 

Simu:255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 



           20 KIVUKONI FRONT,
   P.O. BOX 9000,
       11466 DAR ES SALAAM, 
                                    Tanzania.

 


Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemteua Balozi Rajabu Hassan Gamaha kuwa Balozi wa Tanzania nchini Burundi.

Balozi Gamaha anachukua nafasi ya Balozi Dkt. Mwasi Nzagi ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria.

Kabla ya uteuzi huo Balozi Gamaha alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Uteuzi huo unaanza mara moja.

-Mwisho-
Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
27 Aprili 2015

Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC waanza jijini Harare

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe, Mhe, Simbarashe Mumbengegwi akifungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) unaojadili Mkakati na Mwongozo wa kuelekea Maendeleo ya Viwanda katika Kanda ya SADC. Mhe. Mumbengegwi amefungua mkutano huo jijini Harare, Zimbabwe  huku akiwa na huzuni kubwa kufuatia taarifa ya kifo cha Bregedia Jenereli Hashim Mbita ambaye alitoa mchango mkubwa katika ukombozi  wa nchi za Kusini mwa Afrika. Mhe. Mumbengegwi aliwaomba wajumbe wote wa mkutano kusimama ili kumuombea dua Bregedia Hashim Mbita.



Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda (Mb) wa katikati akiomba dua kumkumbuka Brigedia Hashim Mbita. Kulia kwa Mhe, Kigoda ni Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb) na kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) nao pia wakimuombea dua Brigedia Mbita.

Meza kuu nayo ikimtakia kheri Brigedia Hashim Mbita.

Katibu Mtendaji wa SADC, Bi. Stergomena Tax akitoa hotuba kwa Baraza la Mawaziri wa SADC.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe, Mhe. Simbarashe Mumbengegwi akitoa hotuba ya ufunguzi ya Mkutano wa Baraza la Mawziri wa SADC.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe akiangalia hotuba aliyekabidhiwa na Katibu Mtendaji wa SADC, Bi. Tax mara baada ya kuwasilishwa na Katibu Mtendaji huyo mbele ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC

Kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb); Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Abdallah Kigoda (Mb); Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) wakiwa na Mawaziri wa nchi nyingine katika Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC.


Picha ya pamoja ya Baraza la Mawaziri wa SADC.




Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Abdallah Kigoda (katikati), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (kulia) na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Nchemba wakiwa katika kikao cha maandalizi kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC jijini Harare, Zimbabwe. 

Mhe. Kigoda akiendesha kikao hicho cha maandalizi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Musa Uledi wa kwanza kushoto akitoa maelezo kwa Waheshimiwa Mawaziri juu ya agenda zitakazojadiliwa katika Mkutano wa Mawaziri wa SADC.

Makatibu Wakuu wakiwa katika kikao cha maandalizi. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha.

Wataalamu mbalimbali wakiwa katika kikao cha maandalizi.

Na. Mwandishi wa Wizara ya Mambo ya Nje.

Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wameanza kikao cha siku mbili jijini Harare, Zimbabwe leo kufanya matayarisho ya Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo, utakaofanyika hapo tarehe 29 Aprili, 2015.

Kikao cha Mawaziri, kinachoongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe, Mhe. Dkt. Simbarashe Mumbengegwi, kinatayarisha agenda ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi, ambao utajikita kwenye Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda wa nchi za SADC. Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye mkutano huo, utakaofanyika chini ya Mwenyekiti wa SADC, Rais Robert Mugabe.



Katika kikao cha Mawaziri, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, anawakilishwa na Naibu wake, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim, ambaye aliwasili Harare jana. Washiriki wengine ni Waziri wa  Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Abdallah Kigoda, Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Nchemba, Naibu waziri wa Uchukuzi, Mhe. Dkt. Charles Tizeba na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Gerson Lwenge.



Mbali na mkakati wa maendeleo ya viwanda na mpango wa utekelezaji wake, Mawaziri watajadili Mpango wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Miundombinu na uanzishwaji wa Soko Huria la Utatu baina ya nchi za SADC, EAC na COMESA.

Kikao cha Mawaziri kilitanguliwa na Kikao cha Maafisa Waandamizi, kilichosimamiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajab Gamaha na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Musa Uledi.

Waziri Membe amuenzi Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha Bregedia Generali Hashim Mbita, kilichotokea hivi karibuni katika Hospitali ya Lugalo Jijini Dar es Salaam. Marehemu Brigedia Generali Mbita aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zambabwe pia atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwenye harakati za ukombozi Barani Afrika.
Waziri Membe akimpa pole Mjane wa Marehemu Bregedia Generali Mbita, Bi. Ngeme Mbita  
Mhe. Membe akimpa pole mtoto wa Marehemu Brigedia Generali Mbita Bi. Sheilla Mbitta
Waziri Membe akizungumza na wafiwa 
Waziri Membe akisalimiana na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini mara baada ya kuwasili kwenye  Msiba wa Brigedia Generali Hashim Mbita
Waziri Membe akisalimiana na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zuberi Zitto Kabwe walipokutana kwenye msiba wa Brigenida Generali Mbita 
Waziri Membe akiwa amejumuika  na Waombolezaji wengine kwenye msiba wa Brigedia Generali Mbitta nyumbani kwake Chang'ombe Jijini Dar es Salaam
Waziri Membe akizungumza na waandishi wa Habari juu ya kifo cha Brigedia Generali Mbita. Waziri Membe alimwelezea Balozi Mbita kama kiongozi makini na mwadilifu na pia alikuwa mwanaharakati mahiri ambaye alihakikisha Bara lote la Afrika linakuwa huru.



Picha na Reginald Philip

Waziri Membe apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Japan.

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Bernard K. Membe (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Japan hapa nchini Mhe.Masaharu Yoshida. Hafla hiyo fupi ilifanyika Wizarani tarehe 28 Aprili, 2015
Balozi Mteule wa Japan hapa nchini Mhe.Masaharu Yoshida akimsikiliza kwa makini Waziri  Membe muda mfupi baada ya kukabidhi nakala zake za hati za utambulisho.
Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya Asia na Australasia Bw.Nathaniel Kaaya (mwenye tai nyekundu)  kwa pamoja na Bw.Thobias Makoba, Katibu wa Waziri na Afisa kutoka Ubalozi wa Japan hapa nchini wakifuatilia mazungumzo kati ya Waziri Membe na Balozi Yoshida (hawapo pichani)
Kikao kikiendelea.
Waziri Membe akifafanua jambo kwa Balozi Yoshida huku Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi.Mindi Kasiga (kulia) akinukuu mazungumzo hayo.
 Mhe. Yoshida nae akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho huku Mhe. Waziri Membe na Maafisa wakimsikiliza kwa makini.

Waziri Membe akifurahia jambo na mgeni wake Balozi Mteule wa Japan Mhe. Yoshida.
 Waziri Membe akiagana na Balozi Mteule wa Japan hapa nchini Mhe. Yoshida  mara baada ya kukabidhi nakala zake za hati za utambulisho.

Picha na Reuben Mchome.

Rais Kikwete amkaribisha Rais Clinton (Mstaafu) Ikulu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameambatana na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. Bill Clinton mara baada ya kuwasili Ikulu, na kufanya mazungumzo naye. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.), ambaye pia alishiriki mazungumzo hayo. Rais Clinton yupo nchini kwa ziara binafsi ya siku tatu.  


Rais Kikwete akiwa katika Mazungumzo na Mhe. Clinton. Wa kwanza kulia ni waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe ambaye alishiriki kwenye mazungumzo hayo pamoja na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe. Dkt. Seif Suleiman Rashid (hayupo pichani)



Waziri wa Mambo ya Nje akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. Bill Clinton, Ikulu Dar es salaam, leo tarehe 28 Aprili 2015. 

Picha na Reginald Philip

Afrika yamuaga Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Mama Salma Kikwete, Waziri wa Ulinzi, Mhe. Hussein Mwinyi (wa tatu kushoto), Mkuu wa Majeshi, Generali Davis Mwamunyange na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue ( wa kwanza kushoto) wakisikiliza hotuba ya Waziri Membe (hayupo pichani) wakati wa shughuli za kitaifa za kumuaga Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita zilizofanyika katika Viwanja vya Lugalo Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Aprili, 2015

Waziri Membe akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Serikali wakati wa shughuli za kuaga mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita wakati wa shughuli za kitaifa za kumuaga zilizofanyika katika Viwanja vya Lugalo Jijini Dar es Salaam.
Waziri Membe akimpa pole Mjane wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita, Mama Ngeme Mbita.


Mhe. Membe akimpa pole mmoja wa watoto wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita wakati wa shughuli za kitaifa za kuaga mwili zilizofanyika katika Viwanja vya Lugalo
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Mama Netumbo Nandi Ndaitwah akiwa ameongozana na Balozi wa Namibia hapa nchini, Mhe.....kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita wakati wa shughuli za kitaifa za kumuaga zilizofanyika katika Viwanja vya Lugalo. 
Mhe. Mama Netumbo Nandi Ndaitwah akimpa pole Mjane wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita, Mama Ngeme Mbita. 
Baadhi ya Wawakilishi wa Serikali ya  Msumbiji nao wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Marehemu Generali Hashim Mbita
Waziri wa Ulinzi wa Zimbabwe, Mhe. S. Sekeramayi (kulia)  akiwa pamoja na Mkuu wa Majeshi wa Zimbabwe, Valarios Sibanda (mwenye sare za jeshi) pamoja na Balozi wa Zimbabwe hapa nchini, Mhe. Edzai Chimonyo (katikati) akiwa na Wawakilishi wengine wakitoa heshima zao za mwisho
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya nae akitoa heshima zake za mwisho huku akiwa ameongozana Katibu Mwenezi wa CCM, Bw. Nape Nnauye. 
Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule akiwa ameonozana na Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoa heshima zao za mwisho.
Kiongozi wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa DRC, Mhe. Juma Halfan Mpango akitoa mkono wa pole kwa watoto wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita
Balozi wa Zambia hapa nchini, Mhe. Judith Kapijimpango nae akitoa pole kwa wafiwa
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga nae akitoa mkono wa pole kwa wafiwa.

...........Matukio mengine kwenye shughuli za kuaga mwili wa Marehemu Balozi Mbita

Waziri Membe akisaini Kitabu cha Maombolezo
Sehemu ya Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa yaliyopo hapa nchini wakishiriki shughuli za kuaga mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita
Mwakilishi wa Serikali ya Msumbiji ambaye ni Mwakilishi wa Kamati Kuu wa FRELIMO, Bw. Zaimundo Domingos Pachinuapa akitoa salamu za rambirambi za Serikali hiyo wakati wa shughuli za kitaifa za kuaga mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita


Mwakilishi wa Serikali ya Afrika Kusini ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Nomaindia  Mfeketo akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya serkali yake.
Sehemu ya waombolezaji wakifuatilia matukio
Waziri Membe akiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Mhe. Mama Netumbo Nandi Ndaitwah wakifuatialia hotuba mbalimbali wakati wa shughuli za kumuaga Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita


Viongozi wa Skauti hapa nchini nao walikuwepo kumuaga Brigedia Generali Hashim Mbita
Juu na Chini ni sehemu ya  waombolezaji wakati wa shughuli za kuaga mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita.
Waziri Membe akisalimiana na Mkuu wa Majeshi, Generali Davis Mwamunyange
Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Brigedia Generali Hashim Mbita likiwa limebebwa na Wanajeshi

Picha na Reginald Philip
==============================

SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA MHE. BERNARD MEMBE,
WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
WAKATI WA SHUGHULI ZA KUMUAGA MAREHEMU BRIGEDIA JENERALI HASHIM MBITA, TAREHE 29 APRILI, 2015





Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu;


Mheshimiwa Benjamin William Mkapa;
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda (Mb)
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;


Mama Ngeme Mbita
Mke wa Marehemu;

Watoto wa Marehemu;

Wanafamilia;

Mheshimiwa Hussein Mwinyi
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa;

Jenerali Davis Mwamunyange
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi;


Mheshimiwa Abdulrahman Kinana
Katibu Mkuu wa CCM;


Viongozi Mbalimbali mliopo hapa;

Mabalozi;

Waombolezaji;

Mabibi na Mabwana;



Nianze kwa kutoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Serikali kwa ujumla. Kifo cha Brigedia Jenerali Hashim Mbita ni msiba mkubwa sio kwetu tu hapa Tanzania, lakini pia kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara na bara lote la Afrika. 

Nimelazimika kusimama na kuzungumza mbele yenu kwa kuwa pamoja na heshima kubwa aliyoipata kama mwanajeshi na nafasi zingine kubwa alizowahi kushika, lakini pia Mheshimiwa  Hashim Mbita alitumikia Taifa lake kama Balozi wetu katika jiji la Harare nchini Zimbabwe kuanzia mwaka 2003 hadi mwaka 2006.

Kama ilivyoelezwa, Mheshimiwa Mbita atakumbukwa zaidi kama Katibu Mtendaji wa Nchi za Mstari wa Mbele (Frontline States) kwa miaka 22 akiwa nguzo muhimu katika harakati za kupinga ukoloni na kupigania Uhuru kwa nchi kadhaa za Kusini mwa Afrika. Iliyokuwa OAU na kwa ridhaa ya Mwalimu Julius Nyerere, Ofisi za nchi za mstari wa mbele ziliweka makao makuu hapa Dar es Salaam ambapo Jenerali Mbita aliitumikia kati ya mwaka 1972 hadi hadi mwaka 1994.  

Ni harakati hizi hizi ndio ambazo zimepelekea Mhe. Mbita kupatiwa tuzo ya “Medali ya Sir Seretse Khama”, tuzo ya Umoja wa Afrika ya “Son of Africa” na pia “The Royal Order of Munhumutapa” iliyotolewa na Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe mwaka 2014.

Ingawaje Mhe. Mbita ametutoka lakini Mawazo na uzoefu wake utabaki nasi daima. Kupitia SADC, “The Hashim Mbita Project” ambayo imeandika na kuhifadhi uzoefu, fikra na kazi zake itakuwa ni hazina kubwa ya Mwanajeshi, Mpigania Uhuru na Mwanadiplomasia Mtanzania. Ameiletea heshima nchi yetu na huyu ni Mkombozi wa kweli wa kupigwa mfano.

Tunajivunia utu wake na ndio maana leo, pamoja nasi tunafutwa mchozi na wenzetu.  Naomba kuwatambulisha  kwenu.

·    Kutoka Namibia, Mheshimiwa Netumbo Nandi Ndaitwah, Naibu Waziri Mkuu na pia Waziri wa Mambo ya Nje.

· Uwakilishi kutoka Zimbabwe, Mheshimiwa Dr. Sydney Selelamayi, Waziri wa Ulinzi na Ujumbe wake.

· Uwakilishi kutoka Afrika Kusini, Mheshimiwa Nomaindia Mfeketo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini.

· Kutoka Msumbiji, Mheshimiwa Raimundos Domingos Pachinuapa, Mwakilishi wa Kamati Kuu wa FRELIMO.

Tunashukuru kwa kuweza kujumuika nasi katika msiba huu.

Kwa heshima na taadhima, tunatoa pole kwa familia na Watanzania wote. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Mheshimwa Balozi Brigedia Jenerali Hashim Mbita mahala Pema Peponi.


Amina!



SADC Heads Of State adopt Industrilization Strategy

$
0
0
President of Zimbabwe and Chairman of Southern Africa Development Community (SADC), H.E Robert Mugabe delivers an opening speech at the SADC Extra Ordinary Summit of Heads of State and Government in Harare, Zimbabwe.


Vice President of The United Republic of Tanzania, H.E Dr. Mohamed Gharib Bilal (R) represented President Jakaya Mrisho Kikwete at Summit.

Part of the delegates who attended the Summit listen the official opening statement from Chairman of SADC, H.E Mugabe.

Part of Heads of State and Government who attended the Summit follow up the opening statement. Right is the President of South Africa, H.E Jacob Zuma

A Cultural group entertains the Heads of State and Government and other delegates in the Conference hall. 
The story by Foreign Ministry's Staff.

Heads of state of the Southern African Development Community (SADC) today adopted an Industrial Development Strategy to leverage the region's resources for sustainable development The strategic plan and roadmap was developed by a Ministerial Task Force mandated by the Heads of State last August.
It is a three-phase programme emphasizing efficient use of resources, value edition, diversification and competitiveness to propel the region into a high tech industrial entity by 2063.

The summit directed secretariat to compile the requisite budget and the Ministerial Council to prepare implementation plan. The Heads of State also approved revision of the Indicative Regional Development Plan, which now gives industrial development top priority.Development of infrastructure, including energy, water, roads and railways and ICT is ranked second while peace and security is third, followed by social services.


The President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya Kikwete, was represented by the Vice-President, Dr. Mohamed Gharib Bilal at the Summit, which was attended for the first time by newly elected Presidents Edgar Lungu of Zambia, Philip Nyusi of Mozambique, Hage Geingob of Namibia and Lesotho Prime Minister Pakalitha Mosisili.


The Summit chaired by Zimbabwe President Robert Mugabe was also attended by the President South Africa , Jacob Zuma, King Mswati of Swaziland and Mauritius Prime Minister Anerood Jugnauth.

The Heads of State and Government Further endorsed a plan to inaugurate  the tripartite Free Trade Area (FTA) combining the SADC, EAC and COMESA blocks in June.


They agreed that the creation of a continental FTA earlier scheduled for 2017 be pushed back to 2020.


In her remarks to the Summit, the SADC Executive Secretary, Dr. Stergomena Lawrence Tax, said the Industrial Development Plan would boost the region's gross product and income per capital.
Chairman Mugabe said member states should brace to finance the plan because western countries were unlikely to help. "Those who benefit from our underdevelopment cannot be expected to help us," he said.
He lamented that although SADC countries ranked highly in global mineral and agricultural output, more than two thirds of their population was below the poverty line.


President Mugabe formerly handed over the Regional Peace Training Centre (RPRC) facility to Dr. Tax as part of the Summit opening ceremony.
The facility for the training of military personnel, police and civilians has been donated to SADC by the Zimbabwe government.

SADC Stops for Mbita

$
0
0
President of Zimbabwe and Chairman of Southern African Development Community (SADC), H.E Robert Mugabe (C) here looks sad following the death of Brigadier Hashim Mbita. President Mugabe before, He led the Summit to observe a minute of silence in honor of Brigadier Mbita, reminded the Summit on major activities that Late Brig. Mbita did during liberation struggle of African Continent.

Vice President of The United Republic of Tanzania (red tie), Dr. Mohamed Gharib Bilal with other delegates observe a minute of silence in honor of Brigadier Mbita during SADC Summit in Harare.

The High Table is also silence to remember Brigadier Mbita.


Story by Foreign Ministry' Staff

Heads of State and Government of the Southern African Development Community (SADC), meeting in Harare, Zimbabwe, today paid glowing tribute to the late Brigadier General Hashim Mbita.

The SADC Chairman, President Robert Mugabe, led the Summit in observing a minute of silence in honour of Brigadier Mbita, who was the Executive Secretary of the OAU Liberation Committee for nearly two decades from 1974.


"He supriintended the programme of all liberation groups (from Southern Africa) in Tanzania. He oversaw the formation and organization of the groups, sourcing of materials, programme of training and deployment," recalled Predident Mugabe, who was a beneficiary.

He said they received the news of Brigadier Mbita's passing with "a deep sense of sorrow."
During the last SADC Summit in August, President Mugabe awarded Brigadier Mbita the highest national honour of Zimbabwe, "The Order of Munhumutapa" and 100,000 US dollars for his contribution to the liberation of that country as well as Mozambique, Angola, Namibia, Cape Verde and Sout

Zimbabwe yaipa majengo SADC kwa ajili ya Kituo cha Kufundishia Walinda Amani

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akishuhudia Rais wa Zimbabwe akikabidhi majengo kwa ajili ya mafunzo ya ulinzi wa amani kwa Katibu Mtendaji wa SADC.


Rais wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Robert Mugabe akiangalia Hati Miliki ya Majengo ambayo Serikali ya Zimbabwe imetoa kwa SADC kuwa Kituo cha Kufundishia Walinda Amani. Hati hiyo ilikabidhiwa kwa Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stergomena Tax anayeonekana kushoto. Majengo hayo yapo kwenye kiwanja chenye ukubwa wa ekari 16 ambayo Zimbabwe imetoa bure kwa SADC kama mchango wake wa kuhamasisha amani na utulivu barani Afrika.





Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa azungumza na Mabalozi wa EU, Ujerumani na Ufaransa hapa nchini

$
0
0
Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Mhe. Filberto Ceriani Sebregondi (mwenye tai nyeusi) akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa pili kulia). Wengine katika picha ni Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Malika Berak (kulia kwa Balozi Filberto) na Bi. Eliet Magogo, Afisa Mambo ya Nje
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Sebregondi akiwa na Balozi Berak na Mhe. Egon Kochanke (mwenye tai ya kijani), Balozi wa Ujerumani hapa nchini na Wajumbe waliofuatana nao wakimsikiliza Balozi Mushy ambaye hayupo pichani.
Balozi Sebregondi akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yao na Balozi Mushy (hayupo pichani) huku Balozi Berak na Balozi Kochanke wakimsikiliza.

Picha na Reuben Mchome


Stop Flocking in South Africa, President Mugabe

$
0
0

Heads of State and government of the Southern African Development Community (SADC), meeting in Harare, Zimbabwe yesterday condemned the recent attacks against African migrants in parts of Durban and Johannesburg in South Africa.
The summit meeting was reacting to a briefing by South Africa President Jacob Zuma on the nature of the xenophobic attacks and measures taken by his government to restore peace.

According to a communique issued after the meeting, "Summit commended the measures that the government of South Africa has put in place and resolved to work together to deal with the situation and ensure it does not recur."
The attacks affected the citizens of SADC member countries of Zimbabwe, Mozambique, Malawi, Zambia and Tanzania, which were forced to evacuate their people.

The violence heightened tension between South Africa and its neighbours, some of whom threatened retaliatory measures.
But briefing the media after the summit yesterday, The SADC Chairman, President Robert Mugabe, said the situation should not be blamed on South Africa alone.
He said an virtually unchecked influx of migrants from neighbouring countries was stretching resources to the limit in South Africa, where the majority blacks were living in dire conditions.

"Only the whites are living well there. Our people should not have the instinct to rush to Johannesburg in the false hope that it is heaven," he said.
The SADC Chair said one way to arrest the influx was for SADC member countries to improve their economies and attract their youth to stay and work at home.
Hundreds of Zimbabweans, Malawians, Mozambicans and Zambians were evacuated following the attacks, but millions more, who are largely unskilled, remain in South Africa.

Twenty six Tanzanians were facilitated by the government to return home last week and the Tanzania High Commission in Pretoria is looking for others who may wish to return home. There was no Tanzanian among eight foreigners reported to have been killed in the attacks

President Zuma has been quoted in the media as saying he would address the root causes of the xenophobic attacks, which he said were poverty, unemployment and immigration.

An estimated 53 percent of the South African population lives below the poverty line, according to the United Nations.

(Ends)
 

Arrival of Dr. Bilal in Zimbabwe 

Vice President of the United Republic of Tanzania, H.E Dr. Mohamed Gharib Bilal is received by Tanzania Government Officials when he arrived at the Melkles Hotel in Zimbabwe. Dr. Bilal represented President Jakaya Mrisho Kikwete at the SADC Heads of State Extra Ordinary Summit on Industrialization held in Harare yesterday.

 

High Commissioner of Tanzania to Zimbabwe, H.E Adadi Rajab makes a briefing to the Vice President prior the SADC Summit. On the left is the Minister of Industry and Trade, Hon. Dr. Abdallah Kigoda (MP).

High Commissioner of Tanzania to South Africa, H.E Radhia Msuya contributes a point during a briefing session towards SADC Summit.


Government Leaders and Officials during the briefing session.

 

Rais Jakaya Kikwete apokea hati za Utambulisho za Mabalozi wa Nchi nne Ikulu Jijini Dar es salaam

Balozi Njoolay akabidhi barua ya pongezi kwa Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari

$
0
0
Balozi wa Tanzania, Nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay, alimkabidhi Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari, barua ya pongezi toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete. 
Balozi wa Tanzania, Nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay (kulia) akiwa katika mazungumzo na Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari, mara baada ya kukabidhi barua ya pongezi toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete
Balozi Daniel Ole Njoolay akiendelea kuelezea jambo kwa Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafy Muhammad Buhari mara baada ya kumaliza mazungumzo


====================================

Tarehe 28 Aprili 2015 Balozi wa Tanzania, Nchini Nigeria Mhe. Daniel Ole Njoolay, alimkabidhi Rais Mteule wa Nigeria Generali Mstaafu Muhammadu Buhari, barua ya pongezi toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Jakaya Mrisho Kikwete. 

Rais Mteule Jenerali Buhari alimshukuru Rais Kikwete kwa salamu hizo na kukiri kwamba alikwishapokea simu ya pongezi kutoka kwake mara tu baada ya matokeo kutangazwa. Wakati wa mazungumzo yake na Balozi Njoolay, Generali Buhari aliisifu Tanzania kwa kudumisha amani na utulivu na kusema kuwa anaamini kwamba Tanzania itaendelea kuwa kitovu cha amani na utulivi Barani Afrika. Imetolewa na Ubalozi Tanzania, Abuja

Ubalozi wa Tanzania nchini Malaysia washerehekea Miaka 51 ya Muungano

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Dkt. Aziz Ponary Mlima akiwa  na mkewe Mama Mkola Mlima pamoja na Wafanyakazi wa Ubalozi wakiwapokea wageni waalikwa kwenye maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ubalozi wa Tanzania nchini humo uliandaa sherehe fupi kuuenzi Muungano.
Balozi Mlima akitoa hotuba fupi wakati  wa maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Balozi Mlima akikata keki kuadhimisha miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Anayeshuhudia ni Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo ambaye ni Naibu Waziri wa Biashara ya Kimataifa na Viwanda wa Malaysia, Seneta Deto' Lee Chee Leong.
Juu na Chini ni Wageni waalikwa wakimsikiliza Balozi Mlima (hayupo pichani) alipowahutubia wakati wa maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika  na Zanzibar
Zawadi ya Muungano


Waziri Membe afanya Mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akisalimiana naWaziri wa Mambo ya Nje wa Burundi,  Mhe. Laurent Kavakure walipokutana kwa chakula cha mchana na kufanya mazungumzo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine Viongozi hao walizungumzia masuala ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili
Waziri Membe akimweleza jambo lililomfurahisha Waziri Kavakure
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Laurent Kavakure akizungumza huku Waziri Membe akimsikiliza 
Mazungumzo yakiendelea
Waziri Kavakure akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu mteule wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Hassan Simba Yahya 
Waziri Kavakure akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa  Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Zuhura Bundala.
Mhe. Kavakure akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga
Waziri Membe (katikati) akimtambulisha Waziri wa Maliasili na Utalii (Kushoto) Mhe. Lazaro Nyalandu kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Mhe. Laurent Kavakure. 
Waziri Membe (Wa Nne kutoka Kushoto), Waziri Kavakure (wa tatu kutoka kulia), Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe. Issa Ntambuka (Wa pili kutoka kulia), Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu Mteule Balozi Simba Yahya, (wa tatu kushoto) ni Mshauri wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Balozi Hassan Lukara. 

Picha na Reginald Philip
==============================================

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA


Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 


          

 20 KIVUKONI FRONT,
          P.O. BOX 9000,
   11466 DAR ES SALAAM, 
                     Tanzania.

 



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), leo amefanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Laurent Kavakure jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro. Mhe. Kavakure aliwasili nchini tarehe 03 Mei 2015.

Wakati huo huo, Mhe. Membe ataongoza ujumbe wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenda Burundi siku ya Jumatano tarehe 06 Mei 2015 kufanya mazungumzo na Serikali ya Burundi kuhusu hali ya kisiasa inayoendelea nchini humo.

-Mwisho-
Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
04 Mei 2015


Taarifa kwa Vyombo vya Habari

$
0
0







Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 


           


20 KIVUKONI FRONT,
   P.O. BOX 9000,
       11466 DAR ES SALAAM, 
                                    Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Awamu ya Tatu yenye jumla ya Watanzania 39 kutoka Yemen wanatarajiwa kuwasili nchini tarehe 06 Mei, 2015 ikiwa ni jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwarejesha nyumbani kufuatia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini humo.

Watanzania hao wakiwemo Wanafunzi watawasili nchini kwa Ndege ya Shirika la Qatar namba QR 1349 majira ya saa 1.55 (saa moja) asubuhi.

Kurejea kwa Watanzania hao kutafanya jumla ya Watanzania waliorejea kutoka Yemen hadi hivi sasa kuwa 62 kati ya   Watanzania 69 waliojiandikisha kurudi  huku jitihada za kuwaandikisha wengine zikiendelea kufanywa na Ubalozi wa Tanzania nchini Oman.

Awamu ya kwanza ya Watanzania waliorejea ilihusisha familia ya watu watano huku awamu ya pili ilikuwa na Watanzania 18.

Itakumbukwa kuwa, hivi karibuni Serikali kupitia Waziri wa Mambo  ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe ilitangaza kuwarejesha nchini Watanzania waliopo Yemen kufuatia machafuko yanayoendelea nchini humo.


IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM.
05 MEI, 2015


Balozi wa Uholanzi atembelea Wizara ya Mambo ya Nje.

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb) kulia akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Mhe. Jaap Fredriks ofisini kwake leo.  Mazungumzo hayo yalihusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Uholanzi.

Mazungumzo kati ya Mhe. Naibu Waziri na Mhe. Balozi yanaendelea. Wengine katika picha, kutoka kulia ni Bw. Adam Issara, Anthony Mutafya na Bi. Zulekha Tambwe ambao ni maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim akiagana na Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Mhe. Jaap Fredriks.

Mwakilishi Mkazi wa UNDP atembelea Wizara ya Mambo ya Nje

$
0
0
Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akimkabidhi kitabu kinachozungumzia Hifadhi za Taifa zilizopo nchini Tanzania Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchni, Bwa. Alvaro Rodriguez alipomtembelea ofisini kwake
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy akimwelezea Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchni, Bwa. Alvaro Rodriguez juu ya Kahawa inayozalishwa Tanzania  na Kampuni ya Panone (Panone Fresh Coffee) 
Balozi Mushy akimkabidhi Bwa. Rodrigues Kahawa iliyofungwa vizuri na kampuni ya Panone



Picha na Reginald Philip

Waziri Membe aongoza Mawaziri wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye mazungumzo Burundi

$
0
0
Mhe. Pierre Nkurunziza, Rais wa Jamhuri ya Burundi akisalimiana na kumkaribisha Ikulu Mhe. Bernard K. Membe, Wazairi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kiongozi wa mazungumzo maalaum baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Burundi.



Mhe. Pierre Nkurunziza, Rais wa Jamhuri ya Burundi kwenye mazungumzo na  Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Mhe. Louise Mushikiwabo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda na Mhe. Amina Mohamed, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya.

Viewing all 3230 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>