Quantcast
Channel: Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation
Viewing all 3230 articles
Browse latest View live

Waziri Membe aongoza Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa EAC

$
0
0

Waziri wa Mambo wa Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri  wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kujadili mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi. Kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera 

Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jopo la Watu Mashuhuri wanaofuatilia hali ya usalama nchini Burundi akijadili jambo na Mjumbe wakati wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri uliofanyika kujadili hali nchini Burundi
Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza Waziri Membe (hayupo pichani). 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Louise Mushikiwabo  
 Mkurugenzi Msaidizi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Burundi Bi. Victoria Mwakasege akinukuu yaliyokuwa yakijadiliwa kwenye mkutano.
Mkutano ukiendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe (Mb.) akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba kabla ya kuanza kwa  mkutano wa dharura wa Mawaziri wa Mambo ya Nje 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Mushikiwabo (aliyetangulia), akiongozana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Mhe. Amina Mohammed kuelekea kwenye ukumbi wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Picha na Reginald Philip.
==============================


Waziri Membe aongoza Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa EAC

Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) umefanyika leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuandaa agenda za Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi  wa Jumuiya  hiyo utakaofanyika tarehe 13 Mei, 2015 kujadili hali ya usalama nchini Burundi.

Akifungua Mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa EAC, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) alisema kuwa nchi ya Burundi inapita kwenye wakati mgumu wakati ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu utakaofanyika hivi karibuni, hivyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ameitisha mkutano huo wa dharura kujadili suala hilo na kutafuta ufumbuzi.

Waziri Membe alieleza kuwa, hali ya usalama nchini humo kwa sasa si shwari huku kukiwa na mfululizo wa maandamano ya wananchi na tayari zaidi ya Wakimbizi 50,000 wamekimbilia nchi  jirani ikiwemo Tanzania, Rwanda na Uganda.

“Lengo mojawapo la Jumuiya ya EAC ni kuhakikisha nchi zote wanachama zinakuwa katika hali ya amani, usalama na utulivu hivyo ni wakati muafaka mkutano huu kufanyika” alisisitiza Waziri Membe

Mhe. Membe aliongeza kuwa Mkutano huo ambao umehudhuriwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa EAC yaani Kenya, Rwanda, Burundi na Uganda pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili Taarifa ya Timu ya Watu Mashuhuri (Eminent Persons) walioteuliwa kufuatilia hali ya usalama nchini Burundi kutoka EAC na Jumuiya ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) inayoongozwa na Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Jaji Joseph Sinde Warioba.

Aidha, Mkutano huo pia utapokea na kujadili Taarifa ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje waliotembelea Burundi hivi karibuni kwa ajili ya kupata taarifa za ndani za hali ilivyo nchini humo; Taarifa ya Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Eneo la Maziwa Makuu; Taarifa ya Kamishna wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika na Taarifa ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi.

Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki chini ya Uenyekiti wa Rais Kikwete utafanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Mei, 2015 na utahudhuriwa na Marais wan chi wanachama wa Jumuiya hiyo akiwemo Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Uganda, Mhe. Paul Kagame, Rais wa Rwanda, Mhe. Pierre Nkurunziza, Rais wa Burundi na Mhe. Uhuru Kenyatta, Rais wa Kenya.

Viongozi wengine walioalikwa kushiriki Mkutano huo ni pamoja na Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma ambaye atawakilishwa na Naibu Rais, Mhe. Cyril Ramaphosa, Kamishna wa Umoja wa Afrika, Mhe. Bibi Nkosazana Dlamini Zuma, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ukanda wa Maziwa Makuu, Bw. Said Djinnit; Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR), Prof. Ntumba Luaba, Kamishna wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika na Wawakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU).

-Mwisho-


EAC SUMMIT DISCUSSES THE SITUATION IN BURUNDI 13TH MAY 2015

Rais Kikwete aongoza Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC uliofanyika Dar es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati wa  Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo uliofanyika Ikulu, Jijini Dar es Salaam kujadili hali nchini Burundi. Mkutano huo pamoja na mambo mengine ulilaani vikali jaribio la mapinduzi nchini Burundi na kuzitaka pande zote nchini humo kuhakikisha hali ya uvunjifu wa amani inakoma mara moja. 
Wajumbe wa mkutano wakimsikiliza Rais  Kikwete (hayupo pichani).
Wajumbe mbalimbali wakiwemo Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakimsiki
Wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia kwa makini hotuba ya Rais Kikwete (hayupo pichani).
Mkutano ukiendelea
Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (Watatu  kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Museveni, (aliyeshikilia kofia),  Rais wa Rwanda, Mhe. Poul Kagame, (Wa tatu kulia), Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta (wapili kulia), Naibu Rais wa Afrika Kusini, Mhe.Cyril Ramaphosa (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Bibi Nkosazana Dlamini-zuma
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Simba Yahya (aliyesimama) akijadiliana jambo na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Ladislaus Komba (Kushoto) baada ya mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC kumalizika.
Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji  Joseph Sinde Warioba (Katikati) akizungumza jambo huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bibi. Joyce Mapunjo  pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Bwa. Innocent Shiyo wakimsikiliza 

Picha na Reginald Philip

Waziri Membe afungua Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Bernard K. Membe (Mb) akifungua Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo. Mkutano huo ulifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Mei, 2015. Katika hotuba yake, Waziri Membe aliwahimiza Watumishi wa Wizara kufanya kazi kwa bidii na kwa kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma
 Sehemu ya Wajumbe wa Baraza  wakifuatilia hotuba ya Waziri Membe (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tisa wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Mkutano ukiendelea huku Wajumbe wa Baraza wakiwa makini kumsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Mhe. Waziri Membe akiendelea na hotuba ya ufunguzi wa baraza hilo.
  Sekretarieti ya Baraza hilo wakiendelea na kazi ya kunukuu kile kinachozungumzwa na Waziri Membe kwa kumbukumbu

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya naye akizungumza machache wakati wa Mkutano wa Tisa wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, BibiRosemary Jairo akitoa neno la shukrani kwa Waziri Membe kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza 

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi.Mindi Kasiga ambaye pia alikuwa Mshereheshaji wakati wa mkutano huo
Waziri Membe akiwa kwenye  Picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Wawakilishi wa TUGHE Taifa na Mkoa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa Mhe.Bernard Membe (Mb) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua baraza la wafanyakazi wa wizara ya Nje na ushirikiano wa kimataifa.


Picha na Reuben Mchome


Rais wa Msumbiji kufanya ziara ya kitaifa nchini

$
0
0

Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 17 Mei, 2015 kwa ziara ya Kitaifa ya siku tatu nchini kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mhe. Rais Nyussi atapokelewa na mwenyeji wake Mhe. Rais Kikwete mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Mhe. Rais Nyusi atakagua Gwaride la Heshima na kupigiwa mizinga 21.

Baada ya mapokezi hayo, Mhe. Nyusi atafanya mazungumzo ya faragha na Rais Kikwete yakifuatiwa na mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Msumbiji.

Baadaye siku hiyo ya Mei 17, Mhe. Rais Nyusi atakutana kwa mazungumzo na Mabalozi kutoka Nchi za Afrika waliopo hapa nchini mkutano utakaofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, Jijini Dar es Salaam na kushiriki Dhifa ya Kitaifa itakayoandaliwa na mwenyeji wake Mhe. Rais Kikwete, Ikulu.

Mhe. Rais Nyusi ambaye ataongozana na Viongozi Waandamizi kutoka Serikali ya Msumbiji atahutubia Kongamano la Biashara litakalowakutanisha Wafanyabiashara wa nchi hizi mbili ambalo litafanyika tarehe 18 Mei, 2015 kwenye Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam.

Aidha, siku hiyo ya tarehe 18 Mei, Mhe. Nyusi atapata fursa ya kukitembelea Chuo cha Diplomasia kinachotambulika kama “Tanzania-Mozambique Centre for Foreign Relations” kilichopo Kurasini ambacho kilianzishwa mwaka 1978 kama mradi wa ubia ili kuendeleza mahusiano ya kindugu ya muda mrefu kwa lengo la kutoa mafunzo ya diplomasia na masuala ya kimataifa kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizi mbili.

Mhe. Nyusi atakutana na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini kabla ya kuelekea Zanzibar ambako atafanya mazungumzo rasmi na Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na pia kuzungumza na raia wa Msumbiji waliopo Zanzibar.

Akiendelea na ziara yake hapa nchini, Mhe. Rais Nyusi ataondoka Zanzibar tarehe 19 Mei, 2015 kuelekea Dodoma. Akiwa Mkoani humo atatembelea Makao Makuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuzungumza na Mwenyekiti wa CCM, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, Mhe. Rais Nyusi atalihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye kutembelea Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mhe. Rais Nyusi anatarajiwa kumaliza ziara yake hapa nchini tarehe 19 Mei, 2015 na kuondokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kurejea Msumbiji.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam.
16 Mei, 2015



Rais wa Msumbiji awasili nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku tatu

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameongozana na mgeni wake Rais wa Msumbiji, Mhe. FilipeJacinto Nyusi mara baada ya kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Rais Nyusi ameanza ziara yake ya kitaifa ya siku tatu hapa nchini kuanzia tarehe 17 hadi 19 Mei, 2015.
Rais Kikwete akiwa na Rais Nyusi kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa la Tanzania na Msumbiji zikipigwa kwa heshima ya Rais Nyusi
Mhe. Rais Nyusi akikagua Gwaride la Heshima
Gwaride la Heshima likipita mbele ya Marais
JUU na CHINI: Mhe. Rais Kikwete kwa pamoja na mgeni wake Mhe. Rais Nyusi wakifurahia burudani kutoka kwenye vikundi vya ngoma vilivyokuwepo uwanjani hapo wakati wa mapokezi. Wengine wanaoonekana kwenye picha ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe (mwenye tai nyekundu), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Mhe. Hawa Ghasia na Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. Oldemiro Baloi (mwenye miwani myeusi)
Shamrashamra za mapokezi kama inavyoonekana.




  




Press Release

$
0
0

H.M King Harald V of  Norway
PRESS RELEASE

H.E President Jakaya Mrisho Kikwete of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.M. King Harald V of Norway on the occasion to celebrate the Norwegian Constitution Day on 17th May, 2015.

The message reads as follows: -

“Your Majesty King Harald V,
   The King of Norway,
   Oslo,
   NORWAY.

It is my pleasure and privilege to extend to you, my heartfelt congratulations on the occasion of your country’s Constitution Day.

Norway and Tanzania have been enjoying excellent bilateral relations over the years. It is my strong desire that these ties of cooperation are maintained and strengthened for the benefit of our two countries and peoples.

I would like to take this opportunity to reaffirm Tanzania’s commitment to working with Norway on matters of mutual interest.

Please accept, Your Majesty, my personal best wishes for your continued good health and peace and prosperity for the people of Norway”.

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International

Co-operation, Dar es Salaam


18thMay, 2015

Rais wa Msumbiji atembelea Chuo cha Diplomasia, afungua Kongamano la Uwekezaji na kuzungumza na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini

$
0
0


Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akiwajadiliana jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia (CFR),  Balozi Mwanaidi Maajar  huku Mkuu wa Chuo hicho Balozi Mohammed Maundi akisiskiliza wakati viongozi hao wakisubiri kumpokea Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi alipotembelea Chuoni hapo leo tarehe 18 Mei, 2015 wakati akiendelea na ziara yake ya kitaifa ya siku tatu hapa nchini. Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini, Dar es Salaam kilianzishwa mwaka 1978 kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Msumbiji.
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Balozi Maundi alipotembelea Chuoni hapo wakati wa ziara yake hapa nchini
Balozi Maundi akiwatambulisha baadhi ya Wahadhiri wa Chuo hicho kwa Mhe. Rais Nyusi
Juu na Chini:  Mhe. Rais Nyusi akizungumza na Wahadhiri, Wanafunzi na Wageni mbalimbali alipotembelea Chuo cha Diplomasia (CFR)
Wajumbe wakifurahia jambo wakati Rais Nyusi (hayupo pichani) alipozungumza nao 
Mhe. Rais Nyusi akifurahia zawadi ya picha ya kuchora inayowaonesha Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Msumbiji, Hayati Samora Machel aliyozawadiwa alipotembelea Chuo cha Diplomasia
Rais Nyusi akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Tanzania na Msumbiji pamoja na  Uongozi wa Chuo cha Diplomasia. Kushoto ni  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, Mhe. Hawa Ghasia (wa kwanza kushoto) ambaye ni Waziri anayeongozana nae kwenye ziara hii.
Mhe. Rais Nyusi akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa Chuo cha Diplomasia
Rais Nyusi akiangalia bango linalosomeka "CHUO HIKI KILIKUWA CHUO CHA ELIMU YA JUU KWA WAPIGANIA UHURU WA AFRIKA" ikiwa ni jina la awali kabla Chuo cha Diplomasia hakijaanzishwa.
Mhe. Rais Nyusi akiangalia Jiwe la Msingi la kuanzishwa kwa Chuo hicho



......Rais Nyusi alipozugumza na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini


Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akifurahia kikundi cha ngoma cha Raia kutoka Msumbiji wanaoishi hapa nchini alipowasili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) kwa ajili ya kuzungumza nao.

Sehemu ya umati wa Raia wa Msumbiji wanaoishi hapa nchini wakimpokea kwa shangwe Rais Nyusi alipokutana  na kuzungumza nao wakati wa ziara yake ya kitaifa ya siku tatu hapa nchini


Mhe. Rais Nyusi akizungumza na Raia wa Msumbiji waishio hapa nchini (hawapo pichani)


Mhe. Rais Nyusi akipokea zawadi kutoka kwa mmoja wa Raia wa Msumbiji wanaoishi hapa nchini



......Rais Nyusi aliposhiriki Kongamano la Biashara na Uwekezaji 


Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano kwa ajili ya kushiriki na kufungua rasmi Kongamano la kukuza Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Msumbiji. Wakati wa Kongamano hilo mada mbalimbali kuhusu fursa za uwekezaji baina ya nchi hizi mbili zilitolewa.

Mhe. Rais Nyusi kwa pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Mhe. Christopher Chiza (kushoto) wakifuatilia mada za uwekezaji zilizowasilishwa wakati wa kongamano la kukuza uwekezaji kati ya Tanzania na Msumbiji
Wajumbe waliohudhuria kongamano hilo.








Rais wa Msumbiji awasili Zanzibar.

$
0
0
Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar akitokea Jijini Dar es Salaam,ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kitaifa ya siku tatu nchini Tanzania.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Ali Mohamed Shein akiwa ameongozana na mgeni wake Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi mara baada ya kuwasili katika  Zanzibar leo tarehe 18 Mei, 2015.
 Rais Shein akiwa na Rais Nyusi kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa  zikipigwa kwa heshima ya Rais Nyusi.
 Rais wa Msumbiji Mhe.Nyusi akikagua Gwaride la Heshima wakati wa mapokezi yake. 
 Rais wa Msumbiji, Mhe.Nyusi pamoja na Rais wa Zanzibar Mhe.Dr.Shein wakifurahia burudani ya kikundi cha ngoma wakati wa mapokezi hayo huku Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe.Maalim Seif Sharif Hamad (kulia kwa Rais Shein) na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe.Balozi Seif Ali Iddi (kulia) wakifurahia pia burudani hiyo.
 Rais Nyusi na Rais Shein wakiteta jambo wakati wakiangalia burudani ya ngoma za asili.


Kikundi cha Ngoma kikitumbuiza wakati wa mapokezi hayo

Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt.Ali Mohamed Shein akiwa na mgeni wake Rais wa Msumbiji pale alipomkaribisha Ikulu kwa mazungumzo.


.....Kuelekea Hotelini


 Halaiki ya Wanafunzi waliokuwa wamejipanga barabarani kusherehesha mapokezi ya Rais wa Msumbiji Visiwani Zanzibar.
 Rais wa Msumbiji akiangalia  mmoja wa watumbuizaji anavyopuliza kifaa chake  kwa ustadi mkubwa huku akiwa  amejilaza chini wakati Rais huyo akiwasili hotelini kwake 

Picha na Reuben Mchome

Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi lihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

$
0
0


Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza na pia anakuwa Rais wa kwanza wa Msumbiji kulihutubia Bunge la Tanzania. Katika Hotuba yake nzuri Rais Nyusi iliwasifu Waasisi wa Mataifa ya Msumbiji na Tanzania na kusifia mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi hizi mbili na kuahidi kuimarisha mahusiano katika Siasa na Uchumi. Rais Nyusi alifanya ziara ya kitaifa ya siku tatu ikiwa ni ziara yake ya  kwanza tangu aingie madarakani. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) wa kwanza kushoto mstari wa pili, pamoja na Wabunge wengine wakisikiliza Hotuba kutoka kwa Mhe. Rais Nyusi (Hayupo pichani)


Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Ombeni Sefue (Kushoto) naye akisikiliza Hotuba kutoka kwa Rais Nyusi
Viongozi Mbalimbali wa Serikali wakisikiliza Hotuba ya Mhe. Rais Nyusi Bungeni. 
 Balozi wa Tanzania nchni Msumbiji, Balozi Shamimu Nyanduga (kulia)  naye akiwa bungeni akifuatilia Hotuba ya Mhe. Rais Nyusi.
Mkurugenzi wa Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge Bw. Jossey Mwakasyuka (Wa kwanza kulia), na Maafisa Mambo ya Nje (wa pili Kulia) ni Bw. Khatibu Makenga akifuatiwa na Bw. Mudrick Soraga (wa tatu Kushoto)
Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda akizungumza
Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akipokelewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda alipowasili katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma na kupata fursa ya kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (katikati) ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
Mhe. Rais Filipe Jacinto Nyusi akiwa kwenye Jukwaa Maalum wakati nyimbo za Taifa  zikipigwa.
Kikosi cha Brass Bendi cha Jeshi la Polisi kikipiga Nyimbo za Taifa mara baada ya Rais wa Msumbiji, Mhe. Nyusi kuwasili katika Viwanja vya Bungeni Mjini Dodoma
Makaribisho ya Rais wa Msumbiji, Mhe. Nyusi yakiendelea katika viwanja vya Bungeni.
Rais wa Msumbiji akikagua gwaride la Heshima wakati wa mapokezi yake mjini Dodoma.
Rais wa Msumbiji Mhe. Nyusi pamoja na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete wakiongozwa kuingia Bungeni na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda.
Rais wa Msumbiji Mhe. Nyusi na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakiongozwa na Spika wa Bunge kutoka Nje ya Bunge mara baada ya Kumaliza kulihutubia Bunge.


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika, Bi. Zuhura Bundala (wa kwanza kushoto), Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Bw. Thobias Makoba (watatu kutoka kushoto), na katikati na Bi Talha Mohamed wakiwa Bungeni. 
Rais wa Msumbiji akipokea Picha yenye mwonekano wa Jengo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Spika wa Bunge,  Mhe. Anna Makinda huku ikishuhudiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete (Wa kwanza Kulia).


Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi na Rais Kikwete wakiwa katika picha ya Pamoja na Viongozi wa Serikali na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Picha na Reginald Philip

Tanzania kukuza Ushirikiano na Indonesia

$
0
0
Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari na Diplomasia kwa Umma kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Ndonesia Balozi Esti Andayane, Balozi Kairuki pamoja na mgeni wake walikutana kwa mazungumzo yaliyo jikita katika kukuza Ushirikiano kati ya Tanzania na Indonesia kwenye nyanja mbalimbali za Kiuchumi.   
Balozi Kairuki akimsikiliza Balozi Esti Andayane wakati wa mazungumzo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Bi. Mindi Kasiga (Wa kwanza Kushoto), katikati Afisa Mambo ya Nje Khatibu Makenga na wakwanza kulia ni Dora Lucas Maina akiwa katika Elimu ya Vitendo.
Ujembe ulioambatana na na Balozi Esti Andayane nao wakisikiliza mazungumzo kati ya Balozi Kairuki na Balozi Andayane (hawapo pichani).
Mazungumzo yakiendelea
Picha ya pamoja baada mazungumzo.

Picha na Reginald Philip


MKUTANO NA MKURUGENZI MKUU WA IDARA YA HABARI NA DIPLOMASIA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA INDONESIA

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Habari na Diplomasia ya Umma (Director General for Information and Public Diplomacy) kutoka Wizara ya mambo ya Nje ya Jamhuri ya Indonesia, Balozi Esti Andayane.

Katika mazungumzo yao, Mabalozi hao wamekubaliana kukuza ushirikiano baina ya Indonesia na Tanzania katika nyanja za uchumi.  Balozi Andayane ameelezea utayari wa Indonesia kuendelea kuisaidia Tanzania katika sekta ya Kilimo kwa kutoa fursa za mafunzo kwa ajili ya wataalam wa kilimo nchini.  Tayari Indonesia imeisaidia Tanzania kwa kujenga Kituo cha Utafiti wa Kilimo kilichopo Mkindo mkoani Morogoro. Aidha, katika mazungumzo hayo Balozi Andayane alitoa taarifa kuwa serikali ya Indonesia imeisaidia Tanzania matrekta pamoja na vifaa vyake. Tayari Wizara ya Kilimo imeshughulikia uingizaji wa matrekta hayo.

Kwa upande wake, Balozi Mbelwa Kairuki aliishukuru serikali ya Indonesia kupitia Mkurugenzi huyo kwa misaada mbalimbali wanayotoa kwa serikali ya Tanzania. Pia alishukuru serikali ya Indonesia kwa kuialika Serikali ya Tanzania katika maadhimisho ya miaka 60 ya ushirikiano kati ya bara la Afrika na Asia zilizofanyika Jakarta na Bandung mwishoni mwa mwezi wa nne mwaka 2015. 


Article 14

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Mbelwa Kairuki (Kulia) akimkaribisha na kufanya mzazungumzo na Mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika Mashariki katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Australia, Bi. Henderson. Mazungumzo yao yalijikita katika kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini hususani katika sekta ya Mafuta na Gesi.
Bi. Henderson akielezea jambo kwa Balozi Kairuki.
Wakwanza kushoto ni Bertha Makilage, (Katikati) ni   Bi. Zainabu Angovi, Maafisa Mambo ya Nje na kushoto ni Bi. Juliet Mutayoba ambaye yupo katika mafunzo  ya vitendo Wizara ya Mambo ya Nje.
Mazungumzo yakiendelea.
Picha ya Pamoja

Picha na Reginald Philip


MKUTANO NA BI. HENDERSON, MKURUGENZI WA KITENGO CHA AFRIKA MASHARIKI KATIKA WIZARA YA MAMBO YA NJE YA AUSTRALIA

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia amekutana na kufanya mazungumzo na Bi. Henderson, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Mashariki kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Australia leo tarehe 21 Mei 2015.

Katika mazungumzo yao, waligusia juu ya maendeleo ya maandalizi ya ziara ya Dkt. Kim Hames, Naibu Waziri Mkuu wa Jimbo la Magharibi mwa Australia na Waziri wa Afya na Utalii. Aidha Bi. Henderson aliipongeza Tanzania kwa kuandaa warsha na mikutano ya kutangaza fursa mbalimbali zipatikanazo nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na  uwekezaji katika sekta ya mafuta, gesi na madini ambapo mwaka jana alihudhuria moja ya warsha iliyofanyika jijini Adelaide, Australia.

Kwa upande wake Balozi Kairuki alichukua fursa hiyo kuishukuru serikali ya Australia kwa nafasi za ufadhili wa masomo ya muda mfupi na mrefu katika sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo na Afya.

Kwa kuhitimisha, Balozi Kairuki alimweleza Bi. Henderson juu ya uwepo wa fursa mbalimbali za uwekezaji nchini na kuwasihi wawekezaji kutoka Australia wasisite kuja kuwekeza katika sekta ya madini, nishati na gesi nchini.

Mkutano wa Nne wa Mabalozi kujadili mchango wa Diplomasia ya Tanzania kuelekea Dira ya Maendeleo 2025 waanza

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) na Katibu Mkuu Mteule wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi uliofanyika katika Hoteli ya Ramada, Jijini Dar es Salaam tarehe 25 Mei, 2015. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwasilisha mada kuhusu Mafanikio ya Wizara katika Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi uliofanyika katika Hoteli ya Ramada, Jijini Dar es Salaam tarehe 25 Mei, 2015. 
Mkutano ukiendelea
Sehemu ya Mabalozi wa Tanzania wakimsikiliza Mhe. Membe ambaye haonekani pichani. Kutoka kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Aziz Ponary Mlima, Balozi wa Tanzania nchini Congo, Mhe. Anthony Cheche, Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Mhe. Nassor Mbarouk na Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Mhe. Chabaka Kilumanga.
Mhe. Membe akiwa na Katibu Mkuu, Balozi Mulamula pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule (wa pili kulia) na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Philip Marmo
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Peter Kalaghe akiwasilisha mada kwa niaba ya Mabalozi wa Tanzania Kanda ya Ulaya na Marekani huku Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Ali Saleh (kulia) ambaye aliwakilisha kanda ya Mashariki ya Kati, Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. John Kijazi (kushoto) aliyewakilisha kanda ya Asia na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya aliyewakilisha kanda ya Afrika wakimsikiliza.
Mabalozi wengine wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi wakifuatilia mada wakati wa mkutano wao wa nne. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi Mhe. Wilson Masilingi, akifuatiwa na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Mhe. Mugendi Zoka na Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Deodorus Kamala
Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Mhe. Daniel Ole Njoolay (wa kwanza kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. James Lugaganya (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Mashariki, Bw. Elibariki Maleko (katikati) wakifuatilia mada.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Musa Azan Zungu akizungumza wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi kuhusu jitihada zinazofanywa na kamati hiyo kuhakikisha maslahi ya Mabalozi na Watendaji wote katika Balozi za Tanzania yanalindwa ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao vizuri.
Wakuu wa Vitengo katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nao wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,   Bw. Isac kalumuna  akifuatiwa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Bw. Mathias Abisai na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi, Bw. Lucas Suka
Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Rajabu Gamaha akichangia wakati wa majadiliano ya mada mbalimbali zilizowasilishwa

Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Silima akizungumza wakati wa majadiliano kwenye mkutano wa nne wa mabalozi. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Modest Mero
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akichangia katika mjadala kuhusu kanda ya Afrika
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki akizungumza wakati wa kuchangia mada kuhusu Kanda ya Asia na Australasia. 
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Begum Taj naye akichangia hoja
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) akizungumza wakati wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi. Pembeni yake ni Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Bi. Victoria Mwakasege
Sehemu ya Sekretarieti wakinukuu mazungumzo wakati we mkutano wanne wa Mabalozi
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Aziz Ponary Mlima akichangia mada huku Balozi Cheche na Balozi Mbarouk
Mkutano ukiendelea

Picha na Reginald Philip


Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa EAC kuhusu Burundi kufanyika mwishoni mwa mwezi Mei

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo tarehe 25 Mei, 2015 kuhusu Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2015 kuhusu masuala ya amani na usalama nchini Burundi. Mkutano huo ambao umeitishwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya EAC, Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete utatanguliwa na Mkutano wa Baraza la Mawaziri.
Mhe. Membe akiendelea na mkutano wake na Waandishi wa Habari


Picha na Reginald Philip

RAIS KIKWETE AFUNGUA RASMI MKUTANO WA NNE WA MABALOZI

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano wa Nne wa Mabalozi wa Tanzania nje ya nchi. Mkutano huo umefanyika katika Hoteli ya Ramada Jijini Dar es Salaam ukiwa umebeba Kaulimbiu isemayo "Diplomasia ya Tanzania Kuelekea Dira ya Taifa 2025".
Mhe. Rais Kikwete akizungumza huku Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (katikati) pamoja na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakimsikiliza.
Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mhe. Rais Kikwete (hayupo pichani)
Wajumbe wengine wakiwemo Wakuu wa Vitengo katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifutilia hotuba ya Mhe. Rais Kikwete ambaye haonekani pichani.
Rais Kikwete akiendelea na hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo ambapo pamoja na mambo mengine aliwakumbusha Mabalozi  kuwathamini Watanzania waishio nje ya nchi, kuendelea kusaidia upatikanaji wa misaada ya maendeleo, masoko ya bidhaa za Tanzania, wawekezaji na teknolojia bora 

Mhe. Rais Kikwete akimsikiliza kwa makini Waziri Membe wakati akimweleza jambo kabla ya kuwahutubia Mabalozi
Waziri Membe akijadiliana jambo na Katibu Mkuu, Balozi Mulamula huku Balozi Sefue akisikiliza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Nne wa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi.
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Sekretarieti ya Mkutano wa Nne wa Mabalozi 
Mhe. Rais Kikwete akiwa ameongozana na Balozi Mulamula kuelekea eneo la kupata picha ya pamoja.
Mhe. Rais Kikwete kwa pamoja na Waziri Membe, Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), Balozi Sefue,  Balozi Mulamula, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Simba Yahya, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge, Mhe. Mussa  Zungu, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Paul Makonda wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wote .
Mhe. Rais Kikwete na Viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi Wanawake
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Picha na Reginald Philip

Watumishi Wizara ya Mambo ya Nje wawapokea kwa shangwe Katibu Mkuu mpya na Naibu Katibu Mkuu

$
0
0

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akikabidhiwa ua na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Bi Amisa Mwakawago alipowasili Wizarani mara baada ya kuapishwa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Balozi Simba Yahya naye akipokea ua kutoka kwa Bi. Lilian Mushi mara baada ya kuapishwa.
Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Balozi Mulamula na Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba wakipokelewa na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walipowasili Wizarani hapo baada ya kuapishwa.




Picha na Reginald Philip 

Rais Kikwete awaapisha Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Balozi wa Tanzania Saudia

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha  Balozi Liberata Mulamula kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Balozi Mulamula anakuwa Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke kuongoza Wizara hiyo na kabla ya uteuzi huo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani. Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu tarehe 27 Mei, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi  Mulamula  akisaini Hati ya Kiapo mara baada ya kumwapisha. 
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Mulamula Vitendea Kazi mara baada ya kumwapisha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Balozi Hassan Simba Yahya  kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kabla ya uteuzi huo Balozi Yahya alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu tarehe 27 Mei, 2015.
 Mhe. Rais Kikwete akishuhudia Naibu Katibu Mkuu  mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Yahya  akisaini Hati ya Kiapo mara baada ya kumwapisha. 
Mhe. Rais Kikwete akimpongeza Balozi Yahya mara baada ya kumwapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha, Mhe. Hemed Iddi Mgaza kuwa Balozi  wa Tanzania nchini Saudi Arabia. Kabla ya uteuzi huo Balozi Mgaza alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mkuu  na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu tarehe 27 Mei, 2015.

Rais  Kikwete akishuhudia Balozi  Mgaza  akisaini Hati ya Kiapo mara baada ya kumwapisha.

Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Mgaza Vitendea Kazi mara baada ya kumwapisha.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mulamula, Balozi Yahya na Balozi Mgaza mara baada ya kuwaapisha katika nyadhifa zao mpya
Mhe. Rais Kikwete kwa pamoja  na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Mohamed Gharib Bilal (wa nne kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (wa tatu kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (wa tatu kutoka kulia), Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (wa pili kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mulamula, Balozi Yahya na Balozi Mgaza muda mfupi baada ya kuapishwa.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika Picha ya Pamoja na Balozi Mulamula, Balozi Yahya,  Balozi Mgaza na baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mabalozi wa Tanzania.
Mhe. Rais Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi aliowaapisha pamoja na baadhi ya Wakurugenzi wa Idara za Mambo ya Nje na Watumishi wa Wizara hiyo
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mulamula (kushoto) na mumewe, Bw. George Mulamula (kulia)

Picha na Reginald Philip

Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kikanda akutana Ujumbe wa EU hapa nchini

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Innocent Shiyo (kulia) akizungumza na Naibu Balozi wa Ujerumani hapa nchini Bw. John Reyels  ambaye pia aliongoza Ujumbe wa Jumuiya ya Ulaya (EU), kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Jumuiya hiyo pamoja na masuala mengine yanayohusu Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 29 Mei, 2015.
Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Mhe. Adam Koeler naye akichangia jambo wakati wa kikao chao na Bw. Shiyo na kulia ni Balozi wa Uholanzi hapa nchini, Mhe. Jaap Frederiks.
Wajumbe wengine walioshiriki kikao hicho akiwemo Balozi wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Malika Barak (kulia)
Bi. Upendo Mwasha (kushoto), Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo.
Balozi wa Uholanzi nchini, Mhe. Frederiks akichangia hoja
Mkutano ukiendelea 
Bw. Shiyo akiagana na Balozi Koeler
Bw. Shiyo akifafanua jambo kwa Maafisa walioshiriki kikao kati yake na Ujumbe wa EU



Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akisoma Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake Bungeni mjini Dodoma jana tarehe 29 Mei 2015.
Kutoka kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya, Mkurugenzi wa chuo cha Diplomasia, Mhe. Dkt. Mihammed Maundi wakifuatilia kwa makini hotuba ya bajeti.


Wageni waalikwa wakiwa katika ukumbi wa Bunge wakifuatilia hotuba ya bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri Membe.


Waheshimiwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani nao wakifuatilia hotuba ya bajeti.


Wageni waalikwa wakiwamo wananchi wa jimbo la Mtama la Mhe. Waziri Membe nao wakifuatilia hotuba ya bajeti ya Waziri Membe.


Kundi lingine la Waheshimiwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wakifuatilia hotuba ya bajeti.


Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Cha Diplomasia wakisikiliza Hotuba ya Bajeti liyokuwa inawasilishwa na Waziri Membe, wakiongozwa na Mwalimu wao Bwa. Jambo
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula (Wa kwanza Kushoto), Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Balozi Irene Kasyanju (katikati) na Balozi Filiberto Sebregondi wa Umoja wa Ulaya wakizungumza jambo nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje. 
Mbunge Dkt. Hamisi Kigwangala akimpongeza Waziri Membe baada ya Bunge kupitisha Bajeti wa Wizara yake
Waziri Membe akihojiwa na Paschal Mayala Mukuu wa Kampuni ya PPR
Picha na Reginald Philip






Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akisoma Hotuba ya Bajeti ya Wizara yake Bungeni mjini Dodoma jana tarehe 29 Mei 2015.
Kutoka kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya, Mkurugenzi wa chuo cha Diplomasia, Mhe. Dkt. Mihammed Maundi wakifuatilia kwa makini hotuba ya bajeti.
Wageni waalikwa akiwemo Mke wa Waziri Membe, Mama Dorcas Membe (wa pili kushoto) wakiwa katika ukumbi wa Bunge wakifuatilia hotuba ya bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri Membe.
Waheshimiwa Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani nao wakifuatilia hotuba ya bajeti.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga naye akifuatilia Hotuba ya Bajeti ilipokuwa inawasilishwa na Waziri Membe (hayupo pichani)
Mkurugenzi Mtendaji wa  Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Bw. Elishilia Kaaya na wageni wengine nao wakifuatilia Hotuba ya Bajeti ya Mambo ya Nje ilipowasilishwa Bungeni
Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa uliaoambatana na Mhe. Waziri Membe ukifuatilia hotuba ya Wizara Bungeni.
Sehemu nyingine ya Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwemo Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wakifuatilia hotuba ya bajet ya Wizara.
Wageni wa Mhe. Membe nao wakifuatilia Hotuba 
Ujumbe wa Mabalozi wanao wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakiongozwa na Mkuu wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa DRC, Mhe. Juma Alfan Mpango (kushoto) wakifuatilia hotuba ya Mhe. Membe
Mama Membe (wa pili kushoto) pamoja na Balozi wa Malawi hapa nchini, Mhe.Hawa Ndilowe (wa pili kulia) na wageni wengine wakisikiliza hotuba ya bajeti ya Waziri Membe
Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Cha Diplomasia wakisikiliza Hotuba ya Bajeti iliyokuwa inawasilishwa na Waziri Membe, wakiongozwa na Mwalimu wao Bw. Jambo
Mbunge Dkt. Hamisi Kigwangala akimpongeza Waziri Membe baada ya Bunge kupitisha Bajeti wa Wizara yake
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju (katikati) na Balozi Filiberto Sebregondi wa Umoja wa Ulaya wakizungumza jambo nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje. 
Waziri Membe (Wa kwanza kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Liberata Mulamula, Mbunge wa Simanjiro Mhe. Christopher Ole Sendeka na Katibu wa Waziri, Bw. Thobias Makoba wakifurahia jambo mara baada ya hotuba ya Wizara kupitishwa na Bunge 
Mbunge wa Maswa Magharibi, Mhe. John Magale Shibuda akisalimiana na Afisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Reuben Mchome katika Viwanja vya Bunge
Waziri Membe akihojiwa na Paschal Mayala Mkuu wa Kampuni ya PPR kuhusu mipango ya Wizara katika mwaka wa fedha ujao 2015/2016
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Membe (wanne kutoka kulia) akiwa katika Picha ya Pamoja na wananchi wa Jimbo la Mtama

Picha na Reginald Philip

Viewing all 3230 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>