Quantcast
Channel: Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation
Viewing all 3230 articles
Browse latest View live

Waziri Membe afungua rasmi Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa EAC

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akifungua rasmi Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Mei, 2015. Mkutano huo ambao ni maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC utakaofanyika tarehe 31 Mei, 2015,  pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili taarifa zitakazowasilishwa na Jopo la Watu Maalum wanaofuatilia hali ya siasa na usalama nchini Burundi, Taarifa ya Wanasheria Wakuu kutoka Nchi Wanachama na Taarifa ya Mawaziri waliotembelea nchini Burundi hivi karibuni kwa ajili ya kutathmini hali. Kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera.
Waziri wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb.) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri.
Waziri mpya wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Alain Nyamitwe (katikati) ambaye anaongoza ujumbe wa Serikali ya Burundi kwenye mkutano huo wa Baraza la Mawaziri
Ujumbe wa Uganda ukifuatilia hotuba ya ufunguzi ya Mhe. Membe (hayupo pichani)
Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Mhe. Amina Mohammed (wa pili kushoto) akiongoza ujumbe wa Kenya wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa EAC
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (wa pili kulia mstari wa kwanza) kwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Innocent Shiyo (kushoto) nao wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Mawaziri iliyotolewa na Waziri Membe (hayupo pichani)



Rais Kikwete aongoza Mkutano wa Pili wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa EAC kuhusu Burundi

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa kwanza kulia) kwa pamoja na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museven (wa pili kulia), Rais wa Afrika Kusini, Mhe Jacob Zuma (wa tatu kutoka kulia), Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Alain Nyamitwe (wa tatu kushoto) na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera (wa pili kushoto), wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kabla ya kuanza rasmi kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kujadili hali ya siasa na usalama nchini Burundi. Mkutano huo ulifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2015. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (wa pili kutoka kulia) akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Joyce Mapunjo na  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje (kulia)  nao wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Dkt. Richard Sezibera akisoma maazimio yaliyofikiwa mara baada ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kumalizika.
Kundi la Watu Maalum la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalofuatilia hali ya siasa na usalama nchini Burundi chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Jaji Joseph Sinde Warioba  wakifuatilia mkutano wa Wakuu wa Nchi wa EAC. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini.
Juu na Chini ni Wajumbe mbalimbali wakifuatilia mkutano wa wakuu wa nchi wa EAC
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Radhia Msuya (katikati) akiwa pamoja na Mkurugenzi Msaidizi katika Ubalozi wa Tanzania nchini Burundi, Bibi Victoria Mwakasege nao wakifuatilia mkutano
Maafisa Mambo ya Nje nao wakifuatilia kwa makini mkutano 
Sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini nao wakifuatilia mkutano 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari,  Bw. Assah Mwambene (katikati) kwa pamoja na Afisa Habari wa Sekretarieti ya Maziwa Makuu Bw. Macdonald Mwakasendile (kushoto) wakirekodi matukio 
Rais Kikwete akifuraia jambo na Rais wa Afrika Kusini Mhe. Zuma pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Museveni mara baada ya kumaliza mkutano.
Rais Kikwete akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Bi.Nkoosazana Dlamini-Zuma kabla ya kuanza mkutano. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe akiongozana na Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta tayari kwenda kuanza mkutano wa kujadili hali ya usalama nchini Burundi .
Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula akizungumza jambo na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya,, Bw. Vervaeke.

....Kuwasili kwa viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Mulamula akisalimiana na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyetta akipita kwenye Gwaride la Heshima mara baada ya kuwasili nchini
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Harrison Mwakyembe akimtambulisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa Rais wa Uganda mara baada ya kumpokea Rais huyo alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Rais Museven akipita katikati ya  Gwaride la heshima. 
Balozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini Balozi Radhia Msuya akisalimiana na Rais wa Afrika ya Kusini alipowasili nchini
Picha ya Pamoja baada ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Picha na Reginald Philip


Media Release

$
0
0

 
                                                              


                                                   MEDIA RELEASE

The Joint Meeting of the COMESA-EAC-SADC Tripartite Sectoral Ministerial Committee took place on 29th-30th May 2015 in Dar es Salaam. The purpose of the meeting was to consider progress made in preparation for the Third COMESA-EAC-SADC Tripartite Summit to be held on 10th June 2015.

The Tripartite Summit launched the Free Trade Area in 2011 when SADC took over the chairpersonship and will be handing over the chairpersonship to COMESA at the third Summit scheduled to take place in June, 2015. Negotiations are at advanced stages and the COMESA-EAC-SADC Tripartite Free Trade Area is expected to be launched at Sharm El Sheikh on 10th June, 2015.

When concluded, the Tripartite FTA will encompass 26 Member States, that is, half of the African Continent with a GDP of over US$1.2 trillion that represents over 50% of the Continent’s GDP, and a population of 625 million. When operational, it will become a means for enhancing economic inter-linkages and enabling business environment to unlock regional potentials, scale up productive capacities and competitiveness, stimulating beneficiations and value chains, enhancing technological set-ups. More importantly, the TFTA will also address the issue of overlapping membership that has resulted in a number of challenges for the region’s business and trading community. It is foreseen that the TFTA will constitute an important foundation for the continental free trade area negotiations that will be launched by the African Union Summit in June 2015 towards the realisation of Agenda 2063 of the African Union.

Ministers reiterated the importance of making tariff offers and concluding related negotiations expeditiously. In this regard they decided that MemberStates that had not exchanged tariff offers do so within 6 -12 months and those that have exchanged and are negotiating tariff offers should endeavour to conclude within 12 months. They noted that rules of origin are a crucial element for the TFTA and therefore Member States needed to expedite work to finalise outstanding areas and agree on the Tripartite rules of origin that will be applied in the new TFTA.
The Meeting also endorsed the transitional arrangements on trade remedies that will apply to the TFTA pending the finalisation of a complete Annex in this area. It should be noted that the TFTA Agreement already includes detailed dispute settlement disciplines and a completed Annex on Tripartite Dispute Settlement Mechanism.

It is worth noting that the SADC region has adopted a Strategy and Roadmap on Industrialisation and therefore the incorporation of the pillars on Industry and Infrastructure are important and strategic components for the success of the Tripartite agenda. From a SADC perspective the Industrialisation work programme should result in the economic and technological transformation of the region, engender competitiveness as an active process to move from comparative advantage to competitive edges, reinforce regional integration and ultimately the development and economic prosperity of the Community. SADC would be implementing this strategy jointly with other regional priorities outlined in the Regional Infrastructure Development Medium Term Plan and the Regional Indicative Strategic Development Plan.

The SADC Industrialisation Strategy is anchored on three pillars, namely: Industrialisation as a champion of economic and technological transformation; competitiveness as an active process to move from comparative advantage to competitive edges, and Regional integration and geography as the context for industrial development and economic prosperity. The important features of the Industrialisation Strategy are focused programmes aimed at enhancing economic inter-linkages to unlock regional potentials, scaling up productive capacities and competitiveness, stimulating beneficiations and value chains, enhancing technological set-ups, and improving the business enabling environment. The implementation of the strategy will be underpinned on sound policies and appropriate enabling environment across the Member States.

In the area of ICT, commendable progress has been made in the SADC region with the roll out of Digital Terrestrial Migration equipment given the looming ITU switch-over deadline of 17 June, 2015.

SADC has developed and adopted the Regional Infrastructure Development Master Plan (RIDMP) which defines SADC’s infrastructure development strategy and constitute basis for prioritization of projects, as well as the modus operandi for implementation. The RIDMP constitutes the approved SADC Regional Infrastructure Development Programme and guides the process of selection and implementation of regional infrastructure projects at the level of feasibility assessments, preparation for bankability and investment.   It also constitutes the basis for SADC Member States commitment to a common infrastructure development programme.

NB: For any further information and clarification, SADC Executive Secretary, H.E. Dr. Stergomena Lawrence Tax is available for an interview.


For inquiries: Dr. Charles Mubita 0682994688 

WAZIRI MEMBE AWASIHI WATANZANIA KUTOCHAGUA VIONGOZI WANAOSAKA UONGOZI KWA KUTOA RUSHWA

$
0
0
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Bernard Membe (Mb) akimkabidhi Bi. Shamim Khan tuzo ya heshima ya kujishughulisha na kazi za kijamii hapa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Bernard Membe akipokea tuzo maalumu kutoka kwa Sheikh Ismail Mohamed wakati wa tamasha la kwanza la Kaswida lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa na kudhaminiwa na Kampuni ya Dira ya Mtanzania. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Bernard Membe  akizungumza katika tamasha hilo la kwanza Qaswida, lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa,Mh Membe amewataka Watanzania kusubiri kwa hamu siku ya kutangaza nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu,

Alisema siku hiyo ya Juni 6, wananchi wasikilize nini anataka kuifanya nchi iweze kuondoka ilipo ikiwemo kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo. “Mkae tayari siku hiyo, naamini uongozi mzuri wa nchi ni ule wa kudumisha amani na utulivu na ili nchi iweze kusonga mbele, maadili kwa viongozi ni muhimu,” alisema Waziri Membe.

Mhe.Membe alitumia nafasi hiyo kuwasihi Watanzania kuacha kuchagua viongozi ambao kwa nje, wanajinadi  wana dini, lakini matendo hayaendani na maadili ya  dini zao. Alisema ili mtu aweze kuaminika kuwa ana dini, jamii ifuatilie katika madhehebu yao, hivyo amewasihi wasichague viongozi wanaosaka uongozi kwa kutoa rushwa.

“Msikubali kuwa na viongozi ambao kwa nje, wanaojinadi kuwa na dini kinyume na matendo yao, lazima mchague wenye hofu ya Mungu ambayo husisitizwa na dini zote,” Alisema uongozi wa heshima ni ule unaochukia rushwa ambayo ni adui wa haki, hivyo amewataka wananchi kuwaogopa wapenda rushwa kama ukoma. 
Baadhi ya Washiriki waliohudhuria tamasha hilo.
Baadhi ya Washiriki waliofika kwenye tamasha hilo la kwanza la Qaswida.
Baadhi ya Washiriki waliofika kwenye tamasha hilo la kwanza la Qaswida.
Mmoja wa washiriki wa tamasha la Qaswida kutoka Madrasa ya Nur-Pugu,Samiu Mussa akighani Qaswida mbele ya wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani) waliofika kwenye tamasha hilo,lililodhaminiwa na kampuni ya Dira  ya Mtanzania
Kikundhi cha Qaswida kiitwacho Iqhyau wakighani Qaswida ya maadili
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Bernard Membe (Mb) akipokelewa na wenyeji wake alipokuwa akiwasili katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa,kwa ajili ya kushiriki tamasha la kwanza la Qaswida
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ulamaa Qaswida Promotions ambao ndio waandaji wa tamasha la kwanza la Qaswida,Ustaadh Jumanne Ligopora akimkaribisha mgeni rasmi  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Bernard Membe 
Sheikh Ismail Mohamed akizungumza jambo na Waziri Membe wakati wa tamasha la kwanza la Qaswida lililofanyika jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Kampuni ya Dira ya Mtanzania.
Waimbaji wa Qaswida kutoka kikundi cha Muumini cha Buguruni jijini Dar es Salaam wakiimba kwenye tamasha la kwanza la Kaswida lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa. Tamasha hilo lilidhaminiwa na Kampuni ya Dira ya Mtanzania.

Mabalozi wa Tanzania nchi za Nje wafanya ziara maalum Chuo Kikuu Dodoma.

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga ambaye pia alikuwa Mkuu wa Msafara wa ziara ya  Mabalozi wa Tanzania walipotembelea Chuo Kikuu cha Dodoma akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Prof.Shaaban Mlacha mara baada ya kuwasili chuoni hapo.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Begum Taj akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Prof. Mlacha mara baada ya kuwasili chuoni hapo kwa ziara maalum.
Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Modest Mero akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Prof. Mlacha mara baada ya kuwasili chuoni hapo kwa ziara maalum.
Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma akiwaongoza  Mabalozi wa Tanzania na Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa  mara baada ya kuwasili chuoni hapo kwa ziara maalum.
 Mabalozi wa Tanzania wakisikiliza kwa makini historia fupi ya Chuo hicho kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Chuo Prof. Mlacha muda mfupi baada ya kuwasili chuoni hapo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali wa Wizara ya Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye pia alikuwa Mkuu wa Msafara wa ziara ya Mabalozi, Bi. Mindi Kasiga  akizungumza machache kuwakaribisha Waheshimiwa Mabalozi   kuanza kikao na uongozi wa chuo hicho.
Balozi wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa,  Mhe.Tuvako Manongi akichangia jambo katika mkutano huo.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe.Peter Kalaghe naye akitoa mchango wake wakati wa mkutano huo.
Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. John Kijazi akichangia mada wakati wa mkutano huo. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe.Radhia Msuya na kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe.Philip Marmo
Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu Dodoma Prof. Mlacha ( aliyesimama mbele)akizungumza wakati wa  kikao chake na Mabalozi wa Tanzania walipotembelea chuoni hapo.
Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha Dodoma(aliyenyoosha mkono) akitoa maelezo wakati wa ziara fupi ya kuzunguka Chuo hicho huku Waheshimiwa Mabalozi wakiangalia kwa makini maeneo ya chuo hicho.
Balozi Tanzania nchini Uganda, Mhe. Ladislaus Komba (kulia) na Mhe.Anthony Cheche wakiangalia mazingira na majengo ya aina yake ya  chuo hicho kama yanavyoonekana kwa mbali.
Picha ya Pamoja.
===============

Picha na Reuben Mchome na Reginald Philip.

Balozi Mulamula akabidhiwa rasmi Ofisi

$
0
0
Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberata Mulamula akikabidhiwa rasmi Ofisi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  Balozi John Haule. Kabla ya uteuzi huo Balozi Mulamula alikuwa Balozi  wa Tanzania nchini Marekani na Mhe.  Haule kwa sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya. Makabidhiano hayo yalifanyika Wizarani leo tarehe 01 Juni, 2015.
Balozi Mulamula akizungumza huku Naibu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya, (kulia kwa Balozi Mulamula), Mhasibu Mkuu Bw. Paul Kabale (wa tatu kutoka kushoto), Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Mambo ya Nje, Bw. Mathias Abisai na Afisa Habari wa Mambo ya Nje Bw. Ally Kondo
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Nigel Msangi (wa kwanza kulia), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango Bw. James Lugaganya na  Balozi Haule wakimsikiliza Balozi Mulamula  (hayupo pichani)
Katibu Mkuu, Balozi Mulamula akiwa kwenye Mkutano na baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo mara baada ya kukabidhiwa rasmi Ofisi na Balozi Haule.


Picha na Reginald Philip

Balozi wa China Nchini amtembelea Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akimsikiliza Balozi wa China hapa nchini, Mhe.Lu Youqing alipomtembelea Wizarani leo.
 Balozi wa China hapa nchini, Mhe.Lu akifurahia jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nje Balozi Simba huku Maofisa wa Ubalozi wa China waliofuatana na Balozi wakifuatilia mazungumzo hayo.
 Balozi Simba akisisitiza jambo katika mkutano huo.
 Mkutano ukiendelea huku Maofisa wa Ubalozi wa China hapa nchini wakiendelea kunukuu kile kinachozungumzwa katika mkutano huo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Asia na Australasia Bw.Nathaniel Kaaya (wa pili kushoto) akifuatilia mazungumzo hayo huku Maofisa Mambo ya Nje, Bw. Medard Ngaiza (wa kwanza kulia) pamoja na Bi.Ramla Hamis wakiendelea kunukuu kile kinachozungumzwa.
 Mkutano ukiendelea

Balozi Hamza awasilisha Hati za Utambulisho kwa Mfalme wa Jordan

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Jordani mwenye makazi yake Kairo Misri Mhe. Mohammed Hamza Mohammed akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mfalme Abdallah II wa Jordan
Balozi Hamza akimsikiliza Mfalme Abdallah II mara baada ya kumaliza kuwasilisha Hati za Utambulisho.




Tanzania yachaguliwa Mjumbe Baraza la Shirika la Hali ya Hewa Duniani

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi (mwenye suti nyeusi) akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano Mkuu wa 17 wa Shririka la Hali ya Hewa Duniani unaofanyika Mjini Geneva, Uswisi. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Celestine Mushy (Kulia)
===================================
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TANZANIA YACHAGULIWA KUWA MJUMBE KATIKA BARAZA LA UTENDAJI (EXECUTIVE COUNCIL) LA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI–WORLD METEOROLOGICAL ORGANIZATION (WMO).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi, amechaguliwa kuwa Mjumbe katika Baraza la Utendaji (Executive Council) la Shirika la Hali ya Hewa Duniani–World Meteorological Organization (WMO) kwa kipindi cha miaka minne kuanzia 2015 hadi 2019. Dr. Kijazi amechaguliwa tarehe 4 June 2015 wakati wa Mkutano Mkuu wa Kumi na Saba wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO-Congress wa 17) ulioanza tarehe 25 Mei 2015 na unatarajiwa kumalizika tarehe 12 Juni, 2015 Jijini Geneva, Uswisi.

Kuchaguliwa kwa Dr. Agnes Kijazi kumetokana na jitihada zilizofanywa na Ubalozi wetu wa Kudumu Umoja wa Mataifa wa Geneva na Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambazo kwa pamoja zilisimamia zoezi la kuomba kura kutoka kwa wanachama na kampeni wakati wa uchaguzi. 

Dr. Kijazi ambaye anaongoza ujumbe wa Tanzania katika ushiriki Mkutano huo ambao una washiriki kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Maji na Ubalozi wa Tanzania Nchini Uswisi.

WMO ni Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya hali ya hewa duniani na mabadiliko ya tabianchi. WMO inatekeleza majukumu na maamuzi kuhusu maendeleo ya sayansi ya hali ya hewa na uboreshaji wake ikiwa ni pamoja na kusimamia viwango katika upimaji na utoaji wa huduma za hali ya hewa kwa nchi wanachama.

Hadi wakati wa Mkutano huu huko nchini Uswisi, WMO ilikuwa na nchi wanachama 191. Katika Mkutano huu nchi za Sudan Kusini na Tuvalu zilikaribishwa rasmi kama wanachama wapya wa WMO. Kati ya nchi hizi 191 ni nchi 37 tu ambazo zina wajumbe katika Baraza hilo kuu. Hivyo hii ni nafasi adhimu na heshima kwa Tanzania, TMA na Dr Kijazi ambaye ni msomi mwenye utaalamu wa kutosha akiwa na Shahada ya Uzamivu (Ph.D) katika Sayansi ya Hali ya hewa.

Kazi kuu ya Baraza la Utendaji la WMO, ambalo Tanzania imefanikiwa kuwa mjumbe ni kuchukua hatua zinazostahili, kwa kushirikiana na Katibu Mkuu wa Shirika hilo kutekeleza maamuzi yanayotolewa na Mkutano Mkuu (WMO-Congress) ambao hukutana mara moja kila baada ya miaka minne.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa alielezea sababu ya Tanzania kugombea nafasi hiyo muhimu kuwa ni pamoja na  kuwa ndani ya chombo cha maamuzi na hivyo kushawishi maamuzi yatakayoinufaisha jamii nzima ya kimataifa ikiwemo Tanzania katika masuala ya hali ya hewa ikiwa ni pamoja na kutoa mwelekeo wa kisayansi katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa yanayoendelea katika maeneo mengi Duniani.

Kwa upande wake, Dkt. Kijazi alieleza kuridhishwa kwake na jinsi ambavyo nchi wanachama 190 walivyoridhishwa na utendaji wa Tanzania katika kipindi cha miaka mitatu (2012-2015) ambacho alikuwa mjumbe wa Baraza hili na hivyo kumchagua tena katika kipindi kingine cha miaka minne. “Hii ni heshima kubwa kwa nchi yangu ya Tanzania na ninaahidi kutumia uwezo wangu wote kutekeleza majukumu ya nafasi hii” alisema Dkt. Kijazi.

Imetolewa na: Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam

05 Juni, 2015


Balozi wa China amtembelea Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Balozi wa China hapa nchini, Mhe.Lu Youquig alipomtembelea Wizarani kwa mazungumzo ya kudumisha ushirikiano wa nchi hizi mbili.
 Mkalimani wa Balozi wa China Bi.Wang Fang akisalimiana na Katibu Mkuu 

Balozi wa China hapa nchini, Mhe.Lu Youqing akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Katibu Mkuu, Balozi Mulamula akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Balozi wa China huku Maafisa wa pande zote mbili wakinukuu kile kinachozungumzwa.
 Balozi wa China, Mhe.Lu akifurahia jambo na Balozi Mulamula
Balozi Lu Youqing akisisitiza jambo katika mkutano huo.
 Maafisa kutoka Ubalozi wa China hapa nchini Mr.Dong (kulia), Mr.Lin Liang (katikati) na Bi.Wang Fang wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Balozi Lu.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw.Nathaniel Kaaya (wa kwanza kushoto) kwa pamoja na  Maafisa  Mambo ya Nje, Bw. Medard Ngaiza (wa kwanza kulia) pamoja na Bi.Ramla Hamis wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Balozi Lu (hawapo pichani).

 Picha na Reuben Mchome

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

$
0
0

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Balozi Linda Thomas - Greenfield alipotembelea Wizarani na kufanya mazungumzo yaliyojikita katika kukuza mahusiano kati ya Tanzania na Marekani katika Sekta mbalimbali.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Mark Childress pamoja na ujumbe ulioambatana na Mhe. Thomas - Greenfield nao wakifuatilia mazungumzo.
Balozi Linda akitoa ufafanuzi wa jambo huku Balozi Mulamula akimsikiliza kwa makini. 
Balozi Mulamula (katikati) akimsikiliza Mhe. Linda alipokuwa akizungumza naye kulia ni Afisa Mambo ya Nje Bwa. Lucas Mayenga. 
Mazungumzo yakiendelea
 Balozi Liberatta Mulamula akimlaki kwa furaha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Balozi Linda Thomas - Greenfield wakati alipowasili na kufanya mazungumzo yaliyojikita katika kukuza mahusiano kati ya Tanzania na Marekani katika Sekta mbalimbali.


Picha na Reginald Philip.


Balozi Mulamula akutana kwa mazungumzo na Ujumbe wa EU hapa nchini

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Kiongozi wa Ujumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) hapa nchini, Balozi Filberto Cerian Sebregondi alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Jumuiya  hiyo na Tanzania na pia kujitambulisha kwa Balozi Mulamula ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje. 
Maafisa Mambo ya Nje Waandamizi wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Balozi Sebregondi (hawapo pichani).
Balozi wa Uingereza hapa nchini Mhe. Diana Melrose kwa pamoja na Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Mhe Adam Koeler na Maaafisa wengine  kutoka nchi za EU  wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Balozi Sebregondi.
Balozi Mulamula na Balozi  Sebregondi wakimsikiliza Balozi Melrose akifafanua jambo
Kikao kikiendelea

Picha na Reginald Philip

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje aongoza maadhimisho ya siku ya Taifa la Sweden

$
0
0
Mgeni rasmi kwenye sherehe ya Siku ya Taifa la Sweden, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye makazi ya Balozi wa Sweden hapa nchini. Mhe. Lennarth Hjelmaker (hayupo pichani).
Balozi wa Sweden hapa nchini, Mhe.Balozi Lennarth Hjelmaker akifungua hafla hiyo iliyofanyika usiku wa tarehe 09/06/2015 katika Makazi ya Balozi huyo Masaki Jijini Dar es Salaam.
 Balozi Lennarth akimkaribisha Balozi Mulamula katika hafla hiyo.
 Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Mhe. Filberto Cerian Sebregondi akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula huku Afisa wa Wizara hiyo Bi.Asha Mkuja (kushoto mwenye kilemba).
 Mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hapa nchini Mhe.Balozi Juma Halifan Mpango akisalimiana na Balozi Liberata Mulamula.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Balozi Mulamula (hayupo pichani)
Afisa wa wizara ya Mambo ya Nje Bi.Asha Hemela akifuatilia hotuba ya mgeni rasmi katika hafla hiyo.
Katibu Mkuu Mulamula akiendelea na hotuba yake,kushoto ni Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe.Lennarth 
 Balozi Lennarth  na Katibu Mkuu Balozi Mulamula pamoja na wageni waalikwa wakinyanyua glasi kutakiana kheri katika ushirikiano wa nchi hizi mbili.
 Balozi wa Sweden Mhe.Lennarth  akicheza kwa furaha pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi huo hapa nchini kama ishara ya kufurahia maadhimisho ya siku ya Taifa lao la Sweden sherehe zilizofanyika katika makazi ya balozi huyo Masaki Jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha watoto wa Maafisa wa Ubalozi wa Sweden hapa nchini walioshiriki hafla hiyo kwa wakiimba kwa ufasaha nyimbo za Mataifa ya Sweden na Tanzania.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa   Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na     Waandishi wa abari katika hafla hiyo.

                            ===================
                          Picha na Reuben Mchome.

Watanzania wengine 13 warejea kutoka nchini Yemen

$
0
0
Kiongozi wa msafara wa Watanzania kumi na tatu waliorejea leo nchini wakitokea nchini Yemeni, Bw.Faiz Abdulsheikh Said akizungumza na Mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi.Asha Mkuja wakati wa mapokezi ya Watanzania hao walipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa Shirika la Ndege la Qatar. Serikali imefanikiwa kuwarejesha nchini zaidi ya Watanzania 100  kutoka Yemen baada ya nchi hiyo kukumbwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe. Zoezi la kuwarejesha Watanzania hao linaratibiwa na kusimamiwa na Wizara kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Oman. Watanzania wengine 15 wanatarajiwa kuwasili nchini kesho tarehe 13 Juni, 2015.
Bi. Asha Mkuja akiendelea kupata maelezo kutoka kwa mmoja wa Watanzania hao Mzee Bader Saleh Omar kuhusu hali ilivyo nchini Yemen.
 Mazungumzo yakiendelea
 Mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje Bi.Asha akimsikiliza kwa makini mzee Bader, akimpa maelezo ya hali ilivyo huko Nchini Yemen.
 Watanzania hao wakijiandaa kuondoka ndani ya Uwanja wa Ndege baada ya kukamilisha taratibu zote.

Picha na Reuben Mchome

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje amuaga Balozi wa Brazil aliyemaliza muda wa kazi nchini

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa pamoja na Mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe. Juma Halfan Mpango wakimsikiliza kwa furaha Balozi wa Brazil aliyemaliza muda wake wa kazi hapa nchini, Mhe.Francisco Suarez Luz (kushoto) kabla ya kuanza kwa hafla fupi ya chakula cha mchana iliyoandaliwa kwa ajili ya kumuaga Balozi Luz. Hafla hiyo ilifanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Juni, 2015.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mulamula kwa pamoja na Balozi Mpango wakiendelea kumsikiliza Balozi Luz mara baada ya kuketi tayari kwa kushiriki chakula cha mchana kwa heshima ya kumuaga Balozi Luz.
Meza Kuu wakiwemo Mabalozi kutoka nchi mbalimbali zenye uwakilishi hapa nchini
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mulamula akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kwa ajili ya kumuaga Balozi wa Brazil aliyemaliza muda wake wa kazi hapa nchini, Mhe. Francisco Suarez Luz. Katika hotuba yake alimshukuru Balozi huyo kwa kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili katika kipindi chote alichokuwepo nchini na kumuomba aendelee kuwa Balozi mzuri kwa kuitangaza Tanzania.
Balozi Luz pamoja na Mablozi wengine wakimsikiliza Balozi Mulamula ambaye haonekani pichani
Balozi Luz nae akitoa hotuba yake ambapo aliisifu Tanzania kuwa ni nchi ya amani na kwamba nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika nyanja mbalimbali za maendeleo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mulamula pamoja na Mabalozi wengine wakimsikiliza Balozi Luz (hayupo pichani)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mulamula na Balozi Luz wakigonga glasi kama ishara ya kuutakia heri ushirikiano kati ya Tanzania na Brazil 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mulamula akimkabidhi Balozi Luz zawadi ya picha ya mchoro unaoonesha Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro kama kumbukumbu ya vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania. Anayeshuhudia ni Bi. Felister Rugambwa, Afisa Mambo ya Nje.
Sehemu ya Mabalozi wakishuhudia Balozi Luz akipewa zawadi (hayupo pichani)
Maafisa Mambo ya Nje nao wakifuatilia matukio wakati wa hafla ya kumuaga aliyekuwa  Balozi wa Brazil hapa nchini. Kushoto ni Bw. Leonce Bilauri na Bi. Felister Rugambwa
Balozi wa Namibia hapa nchini akiwa pamoja na Balozi wa Cuba nchini.
Balozi wa Urusi hapa nchini Mhe. Yuri Fedorovich Popov (kushoto) akimweleza jambo mmoja wa wageni waalikwa kwenye hafla ya kumuaga Balozi wa Brazil
Sehemu nyingine ya Wageni waalikwa



Waziri Membe awaaga Mawaziri wa nchin wanachama wa Umoja wa Afrika

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimtaifa, Mhe. Bernard Membe (Mb.) akisoma Hotuba ya kuwaaga Mawaziri wenzake katika mkutano wa Mawaziri wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa (watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe. Naimi Azizi (wa Nne kulia), Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia Balozi Dkt. Mohamed Maundi, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Afrika Bi. Zuhura Bundala pamoja na ujumbe alioambatana nao



Katibu Mkuu Balozi Mulamula apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Qatar nchini

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akipokea Nakala ya Hati za Utambulisho kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kutoka kwa Balozi Mteule wa Qatar nchini Tanzania,  Mhe. Abdullah Jassim Mohamed Al Maadadi leo tarehe 17 Juni 2015.
Balozi Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi Al Maadadi mara baada ya Balozi huyo kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati (wa kwanza kulia) Bw. Elibariki Maleko na Afisa Mambo ya Nje Bwa. Batholomeo Jungu wakisikiliza kwa makini mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Balozi Mulamula na Balozi Mteule Mhe. Al Maadadi (hawapo pichani). 

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Mambo ya Nje aagana na aliyekuwa Mkurugenzi wa UNDP nchini

$
0
0
Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akimkabidhi Kitabu kinachoelezea Vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo nchini Mkurugenzi wa UNDP nchini, Bw. Philippe Poinsot, alipokuja kuaga mara baada ya kupata uhamisho wa kwenda kuwa Mratibu Mkazi wa UNDP nchini Moroco
Balozi Mushy akiwa katika mazungumzo na Bw. Philippe Poinsot mara baada ya kumkabidhi kitabu.
Balozi Mushy (wa nne kulia)  akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Poinsot (wa nne kushoto) pamoja na Maafisa Mambo ya Nje wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa
Picha na Reginald Philip 

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi wa Norway nchini

$
0
0
Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Liberatta Mulamula (Kulia)  akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Norway hapa nchini, Mhe. Hanne Maria Kaarstad. Mazungumzo hayo yalijikita katika kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Norway.
Balozi Kaarstad akimweleza jambo Katibu Mkuu, Balozi Mulamula
Mazungumzo yakiendelea huku Bi. Tunsume Mwangolombe (kulia), Afisa Mambo ya Nje akisikiliza kwa makini.


Picha na Reginald Philip.

Balozi Mulamula akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Sudan nchini

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Baloz Liberata Mulamula  akisalimiana na Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Dkt. Yassir Mohammed Ali alipokuja kumtembelea Wizarani na kufanya nae mazungumzo pamoja na kumpongeza kwa kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje.
Katibu Mkuu, Balozi Mulamula  akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Sudan, Dkt. Mohammed Ali. Kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bi. Talha Mohammed na kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Sudan nchini.
Picha na Reginald Philip

Viewing all 3230 articles
Browse latest View live


Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>